Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, March 4, 2012

Madaktari kutishia kugoma tena, Je wanatumia elimu yao kuleta tija katika jamii


Hivi juzi tu madaktari walitishia kugoma tena kufanya kazi iwapo serikali haitawafukuza kazi waziri wa afya na naibu wake.

Hatua hii imekuja ikiwa ni mwezi mmoja tu tangia Waziri Mkuu Mizengo Pinda kukutana nao na kujadiliana kwa kina masuala ya maslahi yao wakati walipokuwa wamegoma na hivyo waliweza kurudi tena kazini.

Kwa sasa hari imekuwa tofauti kwa kuwa ni keshokutwa tu (Jumatano) ambapo wamesema kuwa watagoma tena kwa kuwa serikai haijawachukulia hatua mawaziri hao.

Je kitendo hicho ni kizuri au ndio hawa madaktari wanataka kutumia elimu yao kuinyanyasa jamii ya watanzania?

0 comments:

Post a Comment