Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, June 23, 2013

Ikiwa bado wiki moja wanafunzi 60,000 wameomba mkopo HESLB

Na Mwandishi Wetu WAKATI ikiwa imebaki wiki moja kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wanaohitaji mikopo kuwa wamewasilisha maombi kabla ya muda wa ukomo, wanafunzi zaidi 60,000 wamejitokeza kuomba kupatiwa mikopo.

 Bodi  ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) katika taarifa yake, imesema mchakato huo ulioanza Mei Mosi mwaka huu na mwisho wa kutuma maombi ni Juni 30. 

Imesema mchakato unaendelea vizuri na  wanafunzi wengi wamejaza fomu za maombi ya mikopo kwa njia ya mtandao. 

Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi ya Wakurugenzi ya Heslb, katika wiki mbili zilizopita,   idadi ya waombaji ilifikia 66,111 miongoni mwao, 424 wakiwa ni waombaji mikopo wa mara ya kwanza waliokwishakamilisha taratibu.  

Wanafunzi 5,320 walikuwa ni waombaji wa mara ya kwanza ambao wako kwenye hatua mbalimbali za ukamilishaji. Aidha wanafunzi wanaoendelea na masomo waliokwishathibitisha kuendelea kupatiwa mikopo kwa mwaka ujao wa masomo ni 60,367. 

 Taarifa hiyo ya Bodi imewataka wanafunzi kuzingatia muda uliopangwa wa kuwasilisha maombi ya mikopo ambao mwisho wake ni Juni 30 mwaka huu.

 Katika mwaka ujao wa fedha, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imetenga Sh bilioni 306 kwa ajili ya mikopo kwa wanafunzi 98,025 wa vyuo vya Elimu ya Juu nchini.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, aliposoma bajeti ya wizara hiyo hivi karibuni, alisema Serikali kupitia Bodi  ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) itatoa mikopo kwa wanafunzi 35,649 ambao ni waombaji wapya na 62,376 wanaoendelea. 

Hata hivyo wanafunzi wanaokidhi vigezo mbalimbali vilivyowekwa na bodi, ndiyo watakaopatiwa mikopo. 

Waziri  Kawambwa katika hotuba yake, alisema mwaka unaomalizika wa 2012/13, wanafunzi 98,773 waliwasilisha maombi na kati yao, 95,594 ndiyo waliopatiwa mikopo. 

 Idadi hiyo ikilinganishwa na wanafunzi  98,025  wanaotarajiwa kupatiwa mikopo mwaka ujao wa fedha,  lipo ongezeko la takribani asili

0 comments:

Post a Comment