Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, June 24, 2012

Zantel yanogesha Epiq Bongo Star Search Zanzibar

 Huyu kijana alikuwa ni mmoja kati ya waliwakuna majaji
 Mkuu wa Mawasiliano wa kampuni ya simu ya Zantel Awaichi Mawala (kushoto) akiimba na wasanii waliokuwa wakisubiria kuitwa ndani kwenye kuimba
Kundi kubwa la watu wakisubiria
                                      
Majaji wakifuatilia shindano hilo ambapo pia walitoa somo la muziki


Na Mwandishi Wetu
UWANJA wa burudani uliopo katika eneo la Ngome Kongwe jana ulifurika maelfu ya vijana waliojitokeza kushiriki katika kinyang’anyiro cha kuchaguliwa kuingia katika fainali za shindano la Epiq Bongo Star Search 2012.

Huku kukiwa na idadi kubwa ya washiriki wasichana pia kulikuwa na washiriki ambao waliwasili wakiwa na vifaa mbalimbali vya kupigia muziki kama vile gitaa,vinanda na vinginevyo ikiwa ni mikakati yao ya kujihakikishia kuchaguliwa.

Akizungumzia usaili wa Zanzibar Jaji Mkuu wa EBSS 2012 Ritha Paulsen alisema kuwa ameguswa na mwamko wa washiriki kutoka Zanzibar.

‘Zanzibar ina vijana wengi wenye vipaji na ambao wanatakiwa kuendelezwa ili kufikia malengo yao katika muziki’ aliongeza Ritha.

Alisema kuwa kupitia shindano la EBSS ambalo linadhaminiwa na kampuni ya simu za mkononi Zantel anatarajia kupata vipaji vingi katika mikoa yote ambayo usaili unaendelea.

Naye Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel kwa Zanzibar Mohamed Mussa mbali na kufurahishwa na idadi kubwa ya washiriki waliojitokeza aliwataka vijana wa kisiwani hapa kutambua kuwa muziki unaweza kuwapatia ajira kubwa.
‘Muziki ni ajira, na ndio maana sisi Zantel tumeamua kuwekeza kwenye mashindano haya ili kuwapa fursa vijana wengi zaidi’ alisisitiza bwana Mussa.




Thursday, June 21, 2012

Tujumuike katika Misa ya kumuombea Issabela Jumamosi ijayo katiak Kanisa la Roman Catholic Makongo Juu


ISABELLA BENITA BULENGO
4TH APRIL 2007 – 24TH APRIL 2012

The family of Mr. & Mrs. James Rugemalira & their beloved daughter Evelyn Rugemalira would like to extend their heartfelt sincere appreciation to all who participated in any way during the funeral arrangements of their beloved granddaughter and daughter, ISABELLA. BENITA. BULENGO (BELLA) who was called on Tuesday, 24th April, 2012  to what is believed by many to be in the Eternal Kingdom of Heaven.  Bella was laid to final rest at her grand parents’ private cemetery in Makongo Juu Dar es Salaam on Saturday, 28th April 2012.
To live in the hearts of others is not to die.  Bella was a child filled with happiness; love;  humility and respect to all she encountered.  She will always live in our hearts.  Let her pray for us to know, love and worship our Lord Jesus Christ better than before by truly living according to the legacy Isabella left behind for us which her grandfather has now proclaimed to be the Bellana inspiration.
There will be a thanks giving mass in Memory of Isabella at the Makongo Juu Roman Catholic Church on Saturday 23rd, June 2012 from 11.30 a.m and thereafter lunch at the Makongo Juu Residence of Mr. & Mrs. James Rugemalira.

Monday, June 18, 2012

Zantel kupitia Epic Bongo Star Search yafanikisha elimu ya muziki kwa wasanii chipukizi

 Mkurugenzi wa Benchmark Production akimpokea mtoto mshiriki huyu aliyefahamika kwa jina la Joha
 Mkuu wa Mawasiliano wa Zantel Awaichi Mawalla akitoa damu kuchangia kituo cha damu cha Dodoma, pia alitoa elimu na kuwasihi vijana kujitokeza kuchangia damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu wenye mahitaji ya damu
 Mshiriki huyu ni mwanafunzi wa kidato cha sita na alijitaidia kuonesha uwezo wake ingawaje hakufikia kiwango na majaji walimpatia elimu ya muziki na kumtaka afanye vema
Hawa walipongezana kwa hatua waliyofikia ingawaje hawakupita lakini walinufaika na elimu ya muziki siku hiyo.


Na Mwandishi wa Elimubora Dodoma
PAZIA la shindano la Epiq Bongo Star Search (EBSS) kwa mkoa wa Dodoma limefungwa rasmi huku vipaji kibao vikiwa vimejitokeza na kuwavutia majaji.

Kilichovutia zaidi ni washiriki wa miaka 16 ambao walionekana kuimba vema na kuwa kivutio hata kwa washiriki wenzao waliofurika katika ukumbi wa Royal Village.

Akizungumzia shindano hilo Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Benchmark Production inayoandaa shindano hilo Ritha Paulsen alisema kuwa amevutiwa na wingi wa washiriki mkoani hapa hasa idadi ya washiriki wasichana pia.

Alisema kuwa ikiwa ni mara ya kwanza kuruhusu washiriki wa miaka 16 kuingia katika usaili wa EBSS 2012 ameshuhudia hazina kubwa ya vipaji  vya washiriki wa umri huo.

Katika usaili huo kulikuwa na washiriki wa aina mbalimbali wakiwamo wanafunzi, wafanyabiashara ndogondogo, vijana wa mitaani na wadau wengineo wa muziki.

Kwa kuthamini umuhimu wa akina mama na watoto mshiriki aliefika kuonesha kipaji chake katika ukumbi huo alipewa nafasi ya kuimba ili aweze kuwahi kuondoka.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Zantel ambao ni wadhamini wakuu wa EBSS 2012  Awaichi Mawalla mbali na kuvutiwa na ushiriki wa vijana waliojitokeza pia alihamasisha upimaji wa damu kwa kuchangia damu kwa kituo cha damu mkoani Dodoma.

“ Kwa kupitia EBSS 2012 tunataka kuwafikia vijana sio tu katika muziki bali pia hata katika kuhamasisha masuala mbalimbali yahusuyo jamii kama vile hili la kuchangia damu na mengineo” alisema Awaichi.

Washindi watakaopatikana watatangazwa baadae katika vyombo vya habari. Baada ya Dodoma kwa sasa inafuata Zanzibar ijumaa ijayo katika eneo la Ngome Kongwe.
Mwisho


Diamond kunogesha Miss Dar Inter College



Na Mwandishi Wetu
MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Nasib Adbdul ‘Diamond’ anatarajiwa kupamba shindano la kumsaka Miss dar Intercollege 2012 linalotarajiwa kufanyika Juni 22 kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa , uliopo mkabala na chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).
Mratibu wa shindano hilo Dina Ismail alisema jana kwamba mbali na Diamond, onyesho hilo pia litapambwa na burudani kutoka bendi ya Skylight iliyopo chini ya mshiriki wa Tusker Project Fame mwaka juzi, Anneth Kushaba.
Alisema maandalizi ya shindano hilo yanakwenda vema ambapo warembo 14 watakaosghiriki  wanaendelea na mazoezi katika hoteli ya  The Grand Villa iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam
“Mwaka huu tumejipanga vema kuhakikisha mmoja ya warembo kutoka Miss Dar Intercollege anafanya vema katika fainali za Miss Tanzania ,”alisema Dina.
Warembo watakaoshiriki shindano hilo  wanatoka vyuo vya  Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ) na Time,  Ustawi wa Jamii,  Usimamizi wa Fedha (IFM)  na Chuo Kikuu huria (OUT ambapo taji linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM, huku mshindi wa pili wa mwaka jana, Blessing Ngowi alitinga fainali za Miss Tanzania.
Dina aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Veronica Ngota, Rose Muchunguzi, Nancy Maganga, Hilda  Edward, Diana Nyakisinda, Neema Michael, Veronica Yollla, Jacquiline Cliff, Sharifa Ibrahim, Natasha Deo, Saada Suleiman, Rose Masanja na Jamila Hassan.

Shindano hilo limedhaminiwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redd’s,Dodoma Wine, Ndege Insurance, Skylight Band,Lamada Hotel, Screen Masters,Makumbusho ya Taifa, Mustafa Hassanali, Shear Illusions, Lamada Hotel,Grand Villa Hotel, Sporti Kizaa zaa, Clouds Fm na blog za Michuzi, Mamapipiro, Bin Zubeiry,Mtaa kwa Mtaa na Fullshangwe.
mwisho
Top of Form
Bottom of Form
Top of Form
Bottom of Form
Top of Form
Bottom of Form
Top of Form
Bottom of Form




Top of Form
Bottom of Form
v

Sunday, June 10, 2012

REPOA na ESRF watoa somo la bajeti kwa kamati za bunge

 Mkurugenzi Mkuu wa Economic and Social Research Foundation, Bohela Lunogelo
 Mtafiti kutoka Taasisi ya Research on Poverty Alleviation (REPOA) Jamal Msami akichangia mada
 Mwenyekiti wa kamati ya hesabu za serikali John Cheyo ambae pia ni Mbunge wa Bariadi Magharibi akizungumza na ofisa habari wa Repoa Hannah Mwandolwa
Mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu(kushoto) mtafiti kutoka Repoa Msami (katikati) na Kongi Lugola Mbunge wa CCM jimbo la Mwigora.

 
Na Mwandishi wa Elimu Bora
SERIKALI imetakiwa kuvitumia vema vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuongeza pato la taifa kutokana na ukusanyaji wa kodi katika vyanzo hivyo.

Rai hiyo ilitolewa juzi na mtafiti kutoka Shirika la Utafiti wa Kuondoa Umaskini (Repoa) Jamal Msami wakati akitoa mada katika semina ihusuyo maandalizi ya bajeti iliyoshirikisha kamati ya bunge ya hesabu za serikali.

Msami alisema kuwa serikali inashindwa kuchangia asilimia kubwa katika bajeti yake ya mwaka kwa kukosa fedha huku ikipoteza asilimia kubwa ya mapato kwa kushindwa kukusanya kikamilifu kodi.

“ Serikali inatakiwa kuhakikisha kuwa inafanya utafiti na kugundua vyanzo vipya vya mapato ambavyo vinaweza kutozwa kodi badala ya kung’ang’ania vyanzo hivyo vilivyopo kila siku huku bado havitoi pato la uhakika” alisema Msami.

Pia alisema kuwa wananchi wanatakiwa  kushirikishwa kikamilifu katika upangaji wa bajeti hiyo ili kushirikisha maoni yao katika bajeti na pia aliwataka wabunge kufuatilia upangwaji wa matumizi ya fedha katika bajeti  hiyo na kujua itakavyowanufaisha wananchi.

Naye Mbunge wa Kilwa Kaskazini Kongi Mangungu alitaka kuongezwa kwa  muda wa kujadili bajeti hiyo kabla ya kuanza kwa kikao cha bunge akisisitiza kuwa muda wa wiki mbili wanaopewa hautoshi.
Pia aliishauri serikali kuweka mkakati utakaosaidia watu kutoka mikoa ya mbali kwenda mijini kutafuta huduma za mbalimbali kwa kuwa asilimia kubwa ya mzunguko wa hela unaamia katika miji hiyo.

Aliongeza kuwa serikali inatakiwa kupunguza misamaha ya kodi inayotoa kwa wawekezaji kwa kuwa inaikosesha serikali fedha ambazo zingesaidia katika bajeti yake.

Bunge la bajeti linaanza kesho huku bajeti ya mwaka huu ikiwa ni trilioni 13 na serikali ikiwa imechangia silimia 40 ya fedha hizo.

.