Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, February 24, 2015

Tigo yawakumbuka walimu Morogoro

Tigo is committed to ensure that teachers in schools and other learning institutions in the country have access to the Internet.

This was said today by the company Interim General Manager, Cecile Tiano, when handing over 50 smartphones provided on credit by Tigo to teachers of Bungo Primary school in Morogoro as a pilot phase of a countrywide initiative by the telecom increase internet access in learning institutions.

As part of the package, the Bungo primary school teachers will also enjoy free access to the internet and making free calls among themselves, Ms Tiano said.

“Apart from creating a seamless communication platform to the teaching staff at the school, we believe that access to the internet will bring new social and economic opportunities to the teachers including e-learning,” Ms Tiano said.

To realize this objective, the general manager said Tigo will continue investing on the expansion and quality improvement of its network infrastructure, noting that the company has already set a side US $ 120 million for this in 2015.

Bungo primary school teachers now join millions of other Tigo customers accessing the company’s online services such as Tigo Music, Tigo Pesa App, free Facebook in Kiswahili and others.

 Ms Tiano said, “This initiative represents our long term commitment to ensure that each and every Tanzanian is able to enjoy and access Tigo internet services and in the process drive a digital transformation agenda in the country.”

Commenting, Bungo primary school headmaster, Roman Luoga, thanked Tigo for the support saying access to the Internet will keep teachers at the school updated and knowledgeable on current issues, not only in the field of academics, but in other spheres of life as well.

“The smartphones and free access to the internet will keep us constantly informed of what is going in our country and the world large hence making us part of the global village,” Luoga said.

Ends


Saturday, February 21, 2015

Chuo cha kwenda ni Eden Hills

HILI NI TANGAZO MAALUM
MKUU WA CHUO
EDEN HILLS COLLEGE - KIBAHA NA MLANDIZI
CHUO BORA TANZANIA CHA DIPOLOMA NA CERTIFICATE KATIKA MASOMO YA BIASHARA, MASOKO,UALIMU,UHASIBU,USHAURI NASAHA,USIMAMIZI WA FEDHA ,UBOHARIA, UANDISHI WA HABARI,UONGO, COMPYUTA, UTAWALA, UTALII, MAENDELEO YA JAMII,MAHUSIANO YA UMMA, MAHUSIANO YA KIMATAIFA NA DIPLOMASIA
SIMU NAMBA
    0715 318 278, 0719 318 278   
Chuo kimesajiliwa na selikalini
NACTE REGISTRATION NO: PWF/060P
TANGAZO LA NAFASI ZA MASOMO Mwaka 2015
DIPLOMA NA CERTIFICATE IN
Business Administration, Procurement and Supply, Information Communication Technology (ICT) na Computer Applications, Accountancy, Marketing,  Human Resource Management , Public Administration , Early Child Hood Teaching, Pre Primary School Teaching , Public Relations , International Relation and  Diplomacy, HIV Counseling, Records Management, Fashion ,Beauty and Designs, Community Development, Tourism Managements, Secretarial Duties, Nursery School Teaching, Journalism and Mass communication, Sales and Marketing ,Wildlife Management, Fashion and Design, Beauty and Modeling, Journalism and Mass Communication, News Righting, Gender, Counseling and Guidance
SIFA ZA KUJIUNGA Na chuo: Kidato cha 4 Na cha 6, VETA au Zaidi.
TUNA PROGRAM MAaLuM ZA:
Evening Classes, Short Course na Distance Leaning
TUNA HOSTEL KWA WAVULANA NA WASICHANA
ADA ni nafuu sana na Kwa awamu au kwa mkupuo
WASILIANA NA MKUU WA CHUO:
0715 318 278, 0719 318 278, 0789 34 34 35 AU 0756 220 978
Email: edenhillscollege15@gmail.com
EDEN HILLS COLLEGE KILELE CHA ndoto yako

Wednesday, February 18, 2015

Haya wale wa ku reseat hii inawahusu

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dk. Charles Msonde.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania anapenda kuwatangazia watu wote wanaotaka kufanya Mtihani wa Kidato Cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) Mwezi Novemba 2015 kwamba usajili umeanza rasmi tarehe 01 Januari 2015.

Watahiniwa watakaojisajili katika kipindi cha kawaida yaani tarehe 01 Januari 2015 hadi 28 Februari 2015 watalipa ada ya Shilingi 50,000/- kwa wanaojisajili mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Shilingi 30,000/- kwa wanaojisajili mtihani wa Maarifa (QT).

Watahiniwa watakaojisajili kwa kuchelewa yaani kuanzia tarehe 01 Machi 2015 hadi tarehe 31 Machi 2015 watalipa ada ya Shilingi 65,000/ kwa Kidato cha Nne na ada ya Shilingi 40,000/- kwa mtihani wa Maarifa (ada pamoja na faini).

 Waombaji wote watajisajili kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya Baraza la Mitihani: www.necta.go.tz. Kabla ya kujisajili kwenye mtandao waombaji watapaswa kwenda kwenye vituo wanavyokusudia kufanyia mtihani kuchukua namba rejea (Reference Number). Wakuu wote wa vituo nchini wamekabidhiwa namba rejea na watazigawa kwa watahiniwa tarajali bila malipo.

Aidha waombaji watapaswa pia kulipa ada ya mtihani kwa njia ya Posta au M-Pesa kabla ya kujisajili kwani hakuna mtahiniwa atakayeweza kujisajili bila kulipa ada ya mtihani.

Waombaji wote wazingatie kwamba kipindi cha usajili kitafungwa rasmi tarehe 31 Machi 2015
Imetolewa Na: KATIBU MTENDAJI

Monday, February 2, 2015

Wanafunzi wakicheza baada ya masomo

Wanafunzi wakicheza mpira wa miguu baada ya kutoka darasani, hapo ni maeneo ya Temeke michezo ni kitu kizuri zaidi kwa wanafunzi lakini bado changamoto iliyopo ni uimarishaji wa Miundombinu bora ya michezo kwa watoto. Maeneo mengi hasa ya mijini hakuna maeneo ya wazi ya watoto kucheza 

Sunday, February 1, 2015

Kipindi cha elimu cha Hatua Jithamini chazinduliwa rasmi

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mawasiliano ya Abel and Fernandez akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Uzuri kuhusiana na kipindi hicho

Mazungumzo yakiendelea

                                          Meneja Masoko wa Cowbell Milk inayodhamini kipindi hicho cha  Luninga, Bertin Mushi
Watoto wakipanga foleni kwenda kujipatia chai ya maziwa ya Cowbell


Watoto wakipata kifungua kinywa kabla ya kuoneshwa kwa kipindi hicho

Watoto wakiangalia kipindi hicho katika ukumbi wa Cinema wa Free Market uliopo Oyster bay

Me pia nikapata wasaha wa kuangalia kipindi hicho ikiwa ni cha kwanza na kitaanza kuoneshwa katika Luninga ya Star Tv na Tv One

Hakika watoto walifurahia kipindi hicho


Fatma na Bertin wakiwa na watoto



Bertin na mwanawe katika picha ya pamoja
Na Evance Ng'ingo
KAMPUNI ya Mawasiliano ya Abel and Fernandez juzi ilizindua kipindi cha Luninga kiitwacho Hatua Jithamini kitakachokuwa kikirushwa na Luninga za Star Tv na Tv One.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya uzinduzi wa kipindi hicho uliofanyikia katika Ukumbi wa Cinema wa Free Market, Oysterbay, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Fatma Fernandez alisema kuwa kipindi hicho kinalenga kuainisha kero, vikwazo na kutoa changamoto kwa mustakabali wa elimu ya Tanzania.

Alisema kuwa kitakuwa ni kipindi chenye kutoa nafasi kwa watu mbalimbali kuzungumzia masuala mbalimbali ya elimu na tayari wamekwisha tembelea mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Tabora, Mwanza, Dodoma, Morogoro, Iringa, Songea na Mtwara kuzungumza na wananchi kuhusiana na changamoto za elimu.

Alisema kuwa kipindi hicho cha dakika 30 kitakuwa kikirushwa kila Jumamosi na Jumapili na kuwataka watanzania kufuatilia ili kutoa mawazo yao kuhusiana na nini kifanyike katika kuzikabili changamoto za elimu nchini

"Kwa hapa nchini, matokeo ya mtihani wa darasa la saba kwa mwaka jana yametoa ishara ya kuimarika elimu yetu huku ufaulu ukiongezeka kwa asilimia 6. Lakini, licha ya ongezeko la ufaulu huo bado wanafunzi waliopata alama dhaifu walikuwa zaidi ya asilimia 43 ya wanafunzi wote. Hili ni moja ya changamoto ambazo nadhani tunapaswa kuifanyia kazi kwa nguvu zote" alisema Fatma.

Aliongeza kuwa "sekta ya elimu hapa nchini, kama zilivyo sekta nyingine inakabiliwa na changamoto nyingi sana lakini ni Imani yangu kuwa tukishirikiana kwa pamoja na tukiwa na mikakati iliyo bora, changamoto hizi hazitakuwa kikwazo cha ustawi wa elimu yetu".

Kwa upande Meneja Masoko wa Cowbell Milk inayodhamini kipindi hicho cha Luninga, Bertin Mushi alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa elimu hasa ya msingi nchini Cowbell imeamua kudhamini kipindi hicho kwa kuwa nao wanasaidia elimu kwa kuwajengea afya watoto kupitia maziwa yao ya Cowbell.
==============

Unesco yateta na wanafunzi wa Buhangija

DSC_0162
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimsikiliza kwa makini Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi aliyekuwa akimwelezea changamoto mbalimbali walizonazo shuleni hapo.(Picha na Zainul Mzige).
Na MOblog, Shinyanga
SHULE ya watoto wenye ulemavu ya Buhangija Jumuishi inakabiliwa na changamoto kubwa zinazofanya maisha kwa watoto hao kuwa magumu.
Miongoni mwa changamoto hizo ni kukosekana kwa huduma za matibabu, walimu wa kutosha na mabweni.
Hayo yamebainika wakati wa ziara fupi ya Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues.
Mkuu wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi, ndiye aliyeelezea ugumu uliopo katika shule hiyo yenye wanafunzi 209 wenye ulemavu wa aina mbalimbali.
DSC_0173
Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi akimtambulisha Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefanyia ziara fupi akiwa safarini kuelekea jijini Mwanza akiwa ameambatana na Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias (katikati).
Alisema shule hiyo yenye walemavu wa aina tatu wa kusikia, ngozi na wasioona inakabiliwa pia na lishe duni ambayo haimpi kijana nafasi ya kuendelea, kwani wanakula mlo wa aina moja na kidogo.
Shule hiyo ambayo awali ilikuwa inawapokea wanafunzi wasioona sasa inapokea walemavu wa ngozi kutokana na hofu iliyokuwa inalikumba taifa ya mauaji ya albino.
Aidha mwalimu huyo alisema kwamba wameiomba serikali kuwa na muuguzi na daktari katika makazi hayo lakini mpaka sasa hawajapatiwa kutokana na wao wenyewe kutokuwa na uwezo wa kuwalipa.
Alisema kutokana na rika mbalimbali na tatizo la walemavu wa ngozi shule hiyo ambayo sasa imegeuzwa kuwa makazi inastahili kuwa na daktari na mabweni yaongezwe.
DSC_0191
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues ( wa pili kushoto) akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga (hawapo pichani) alipofanya ziara fupi akiwa safarini kuelekea jijini Mwanza akiwa ameambatana na Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias (wa pili kulia). Kulia ni Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi.
Aidha mwalimu alisema walimu kwa ajili ya viziwi hawatoshi.
Naye Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues, amesema ameyaona mazingira hayo na kuahidi kushirikiana na marafiki na mamlaka nyingine kuboresha mazingira ya kituo hicho.
Alisema kwamba amefurahishwa kuwapo katika kituo hicho na kuona namna wanavyoweza kusaidia sehemu hiyo ya jamii kutojisikia upweke.
Akizungumza na watoto hao walimwambia kwamba wana changamoto ya nguo, vitanda, vitabu na mahitaji mengine ya lazima kama watoto na wanafunzi.
DSC_0177
Baadhi ya watoto wanaosoma shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga wakimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (hayupo pichani).
DSC_0201
DSC_0222
Mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Loreto mkoani Shinyanga Beatrice Leme anayelelewa kwenye kituo hicho kutokana na kukithiri kwa mauaji ya walemavu wa ngozi mkoani humo akimwelezea changamoto mbalimbali zinazowakabili kwa niaba ya wanafunzi wenzake Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefanya ziara fupi shuleni hapo.
DSC_0233
Mwanafunzi wa darasa la sita shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga, Daniel Limbu akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues kwa niaba ya wanafunzi wenzake.
DSC_0256
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues, Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias pamoja na Mkuu wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi wakifurahi pamoja na watoto wenye ulemavu wa ngozi katika shule hiyo.
DSC_0257
DSC_0301
Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi wanaolelewa kwenye kituo hicho ambacho ni salama kwao kutokana na hofu iliyokuwa inalikumba taifa ya mauaji ya albino.
DSC_0274
Baadhi ya majengo ya mabweni ya shule ya msingi Buhangija ya wilayani Shinyanga.
DSC_0306
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi wakicheza mpira kwenye mazingira salama shuleni hapo kutokana na hofu iliyokuwa inalikumba taifa ya mauaji ya albino.
DSC_0308
Mkuu wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi akimtambulisha mtoto Erick mwenye ulemavu wa ngozi kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kushoto) aliyefanya ziara fupi kwenye kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu (mahitaji maalum).
DSC_0322
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimsuka kwenye bembea mmoja wa watoto wenye ulemavu wa ngozi Zawadi Deus anayesoma shule ya msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga wakati wa michezo alipofanya ziara fupi shuleni hapo.
DSC_0358
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akisaini kitabu cha wageni wakati akijiandaa kuondoka shuleni hapo baada ya kuhitimisha ziara yake fupi. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi.
KAWAIDA

Binti albino alietekwa apatikane == UNDP

DSC_0019
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akimtambulisha Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati) alipoitishia mkutano na waandishi wa habari jijini Mwanza mara baada kuhitimisha ziara zake Kanda ya ziwa. Kushoto ni Mshauri wa masuala ya haki za binadamu kutoka ofisi ya mratibu mkazi wa UN Tanzania, Bi. Chitralekha Massey.
Na Mwandishi wetu, Mwanza
MRATIBU wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la maendeleo la Umoja huo, UNDP, Alvaro Rodriguez ameutaka uongozi mkoa wa Mara kuanzia Polisi hadi serikali ya mkoa kuweka kipaumbele kumtafuta binti albino ambaye ametekwa na watu wasiojulikana siku 14 zilizopita.
Hayo aliyasema jana kwenye mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jijini
Mwanza baada ya kutembelea mkoa ya kanda ya ziwa ikiwemo Mara, Shinyanga na Mwanza kuangalia miradi inayotekelezwa na Umoja wa Mataifa pamoja na masuala ya haki za binadamu.
Alisema serikali kupitia Mkuu wa mkoa na Kamanda wa polisi mkoa wahakikishe wanaendelea kumtafuta na kulipa suala la Pendo Emmanuel (4) kipaumbele .
Pendo alitekwa na watu wasiojulikana baada ya mlango wa nyumba yao kuvunjwa Desemba 27,2014 kwa jiwe la fatuma katika kijiji cha Ndami tarafa ya Mwamashinda,wilayani Kwimba mkoani hapa ambapo hadi sasa bado hajapatikana.
Aidha aliwataka wananchi na viongozi kuhakikisha usalama wa watu wenye ulemavu kwani wao ni binadamu kama binadamu wengine na wanahitaji haki yao ya msingi ya kuishi bila hofu na manyanyaso kutoka kwa jamii inayowazunguka.
Mwakilishi huyo wa Umoja wa mataifa alisema katika mkutano huo kwamba hata kurundikana kwa watoto walemavu wa ngozi katika kituo cha Buhangija kilichopo Shinyanga ni matokeo ya mauaji yanayoendeshwa dhidi yao na kusema suluhisho la tatizo hilo ni jamii kuwakubali watu wenye ulemavu wa ngozi.
Tayari watu 15 wanashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi wa kuhusika na uporwaji wa mtoto huyo akiwemo baba mzazi, Emmanuel Shilinde.
Pamoja na kuzungumza na waandishi wa habari mkoani Mwanza, kuelezea ziara yake katika Ukanda wa Ziwa, Mwakilishi huyo pia alizuru wilaya ya Magu na kukagua mradi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ,UNICEF, wenye lengo la kuhakikisha haki inatetendeka dhidi ya wale wanaonyanyasa watoto na haki zao za kibinadamu zinahesmiwa.
DSC_0095
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza.
Akiwa Magu alifurahishwa na mashikamano unaoneshwa na serikali na wadau wengine kuhakikisha kwamba mradi huo unafanikiwa hasa katika kuwezesha watu kutambua haki za msingi za watoto na kutoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto waliofanyiwa unyanyasaji na kuanzishwa kwa dawati la watoto na jinsia vituo vya polisi.
Hata hivyo aliambiwa changamoto zinazoambatana na ukusanyaji wa taarifa hasa katika maeneo ya ndani zaidi.
Katika mazungumzo yake na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magese Mulongo, Umoja wa Mataifa na Serikali ya Mkoa walikubaliana kwamba usalama wa wananchi hasa watoto nay ale makundi maalumu ndio suala la msingi ambalo pande zote hizo mbili itatilia maanani.
Akiwa Shinyanga, Mwakilishi huyo Alvaro Rodriguez nalea kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa ngozi , wasiiona na viziwi Buhangija na kujionea hali halisi ya mrundikano wa watoto.
Kituo hicho kina watoto 220 wenye ulemavu wa ngzoi ambao walikimbiziwa hapo baada ya usalama wao kuwa shakani.
Alifurahishwa na juhudi zinazofanywa na wadau mbalimbali kuimarisha hali ya ustawi katika kituo hicho ambacho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za mrundikano wa watoto, afya na lishe.
DSC_0080
Mkutano na waandishi wa habari uliotishwa na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez ukiendelea.
Alisema akiwa hapo kwamba kama sehemu ya ajenda ya Umoja wa mataifa kusaidia kulinda haki za binadamu na kuhakikisha wale wanaoishi na ulemavu wa ngozi wanaendelea kustawi na haki zao zinaoheshimiwa, mwakilishi huyo alisema Umoja wa Mataifa utaendelea kutoa msaada kwa kundi hilo.
Pia alifanya mazungumzo na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na mkuu wa wilaya hiyo Anna Rose ambapo walikubaliana kwamba suluhu ya mwisho ni kwa watanzania kuwakubali wenye albinizim kama wenzao na kuacha kuwatafuta kuwaua kwa imani za kishirikina.
Akiwa mkoani Mara alishiriki katika hafla ya kutunuku vyeti wasichana na wavulana waliofuzu mafunzo ya miezi miwili yenye lengo la kuwaingiza katika jamii bila kukutwa au kufanyiwa tohara yenye maumivu (kwa wavulana).
Mafunzo hayo ni mchango wa Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la UNFPA wenye lengo la kukabiliana na mila potofu ikiwamo ya ukeketaji na mimba za utotoni zinazotokana na mabinti kuolewa wakiwa wadogo.
Katika mazungumzo na mkuu wa mkoa wa Mara, kapteni mstaafu Asery Msangi, Umoja huo ulikubaliana na serikali ya mkoa kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha haki za msingi za binadamu zinaheshimika na wananchi kuelimishwa kuhusu haki hizo.
KAWAIDA