Help Children
Love them
Saidia Watoto

Friday, September 27, 2013

Elimu kupinga ugaidi ianzie ngazi ya chini

Askari akiwakoa watu waliokuwa kwenye Mall hiyo
 HIVI karibuni nchini Kenya katika jiji la Nairobi kulitokea tukio kubwa na la kusikitisha lililohusisha magaidi wa kundi la El Shabab kuvamia na kuua watu wasiokuwa na hatia waliokuwa kwenye Mall ya West gate nchini humo.

Tukio hilo la aina yake limegusa nyoyo za watu wengi duniani kote hasa ikizingatiwa kuwa wapo watu mbalimbali wakiwamo wanawake na watoto wameuwawa katika tukio hilo.


Mauaji hayo ni ya kinyama ambayo yanatakiwa kutufumbua macho wanajamii katika kuangalia namna mpya ya kukabiliana na matukio kama hayo.


Hakika njia mojawapo kubwa ya kupambana na matukio kama haya ni kwa njia ya kutoa elimu ya kutosha katika kupambana na hali hiyo.


Zipo elimu kwa njia ya filamu ambazo zimetolewa ambapo wacheza filamu wa mataifa mbalimbali wamekuwa wakielimisha vita dhidi ya tukio hilo.


Lakini pia zipo elimu kwa njia za nyimbo ambapo wasanii wamepiga vita kwa kuonesha athari za matukio kama hayo pia.


Kwa sasa harakati za kuelimisha watu kuhusiana na ubaya wa ugaidi ziingie  katika ngazi mbalimbali za elimu hasa sekondari, hapa nikiwa namaanisha katika somo kama Civics.


Hii itasaidia kwa kiasi fulani kuwaweka watu tayari katika ufahamu wa matukio kama hayo ambayo ni yameshaanza kuwa hatari kwa usalama wa mataifa ya Afrika Mashariki.

Wanafunzi wakielimishwa wanaweza kuwaelimisha watu mbalimbali katika jamii na hatimae kushiriki kikamilifu katika kupambana na hali hiyo.


Ifikie wakati hata elimu hiyo ielezee namna bora ya kupambana na ugaidi huo hasa katika kuwajibika kwa kuwafichua watu katika jamii ambao wanahisi kuwa sio wema.


Ni muda sasa kwa Tanzana kuliangalia suala hili katika umakini wa hali ya juu na kujipanga ili kuhakikisha kuwa hawa watu hawaingii hata kidogo na kufanya ubaya huku kwetu.


Elimu hii ikiendelea itasaidia wanajamii nao kutambua ubaya wa watu hawa na kamwe kutowaunga mkono.


Kwa sasa utakuta basi hasa daladala zina picha za Osama au utakuta limeandikwa jina la kundi la El Shabab sasa hio sio nzuri kwa kuwa ni kama linaongeza hamasa ya ugaidi.


Ni matumaini yangu kuwa kila mtanzania analiona tukio la ugaidi kuwa ni lake na lipo karibu yake na hivyo ana nia ya dhati katika kupambana nalo.


Blog hii inaribisha mawazo yanayohusiana na utoaji wa elimu dhidi ya ugaidi.
Mwandishi wa hili wazo ni
Evance Ng'ingo
0714 43 65 94


Wednesday, September 25, 2013

Mengi ya kujifunza katika tamasha la Sanaa Bagamoyo

Msanii maarufu hapa nchi wa muziki wa kisasa Misoji  Nkwambi   wa katika  wa kushoto ni mwanachuo  Safina Amani na wakulia ni Clement Chares akicheza ngoma na hivi sasa misoji ni mwanachuo wa chuo cha sanaa bagamoyo .(Picha kwa Hisani ya Simon Makala, Mwanamakala blogspot.com).


“WANACHUO TUNACHEZA HIVI’
wanachuo wa chuo cha sanaa bagamoyo wakicheza ngoma kwenye tamasha la sanaa la kimataifa linalofanyika katika viwanja vya chuo cha sanaa bagamoyo wakionyesha umahili wao wa kuisakata ngoma .mbele ya mgeni rasimi jana katika ukumbi wa chuo bagamoyo mkoani pwani. (Picha kwa Hisani ya Simon Makala, Mwanamakala blogspot.com)

watoto wadogoGozibet Bwere miaka minne na mwingine  Nyambuli Aginess Muganga wa kikundi cha ngoma cha Utandawazi  Theater Group Matwigachallo, kutoka kijijij cha Nansore Wilaya ya ukerewe mkoa wa mwanza wakiwa wanacheza ngoma jana katika ukumbi wa chuo cha sanaa Bagamo kwenye Tamasha  la kimataifa la  32la sanaa na Utamaduni Bagamoyo, kauli mbiu ni sanaa na utamaduni katika kukuza Utalii linalo endelea katika chuo cha sanaa bagamoyo mkoani Pwani. .(Picha kwa Hisani ya Simon Makala, Mwanamakala blogspot.com)
 

“WANACHUO TUNACHEZA HIVI’
wanachuo wa chuo cha sanaa bagamoyo wakicheza ngoma kwenye tamasha la sanaa la kimataifa linalofanyika katika viwanja vya chuo cha sanaa bagamoyo wakionyesha umahili wao wa kuisakata ngoma .mbele ya mgeni rasimi jana katika ukumbi wa chuo bagamoyo mkoani pwani. (Picha kwa Hisani ya Simon Makala, Mwanamakala blogspot.com)
Na Mwandishi Wetu

NAIBU WAZIRI AMOSI MAKALA; “ Sanaa na utamaduni kuleta ajira”
 
Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo
 
NAIBU  Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amos Makala  amesma Sanaa na Utamaduni nchini itaendelea kuenziwa ili kuwaleta ajira vijana pindi watakapokuwa tayari kuienzi kwa vitendo na kuisomea.
 
Makala alisema hayo mjini hapa alipokuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa tamasha la 32,  la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lenye kauli mbiu ‘Sanaa na Utamaduni katika kukuza utalii’ linaloshirikisha vikundi zaidi ya 70, kutoka ndani na nje ya Tanzania.
 
Akihutubia, umati wa wananchi,wanafunzi wa chuo hicho cha sanaa na vikundi mbalimbali vinavyoshiriki, Waaziri Makala alisema akiwa waziri mwenye dhamana atahakikisha utamaduni na sanaa nchini inakua huku ikiwanufaisha watu wote kwa vizazi vya sasa  na vya baadae.
 
“Katika kuenzi  Sanaa na Utamaduni, Wizara ina mipangilio mingi ikiwemo nay a kuakikisha tunakuza utamaduni wa Taifa letu na hata ajira kwa vijana ambao watajiunga na sanaa hivyo tutaendelea kushirikiana na chuo cha TasuBa  na wadau wengine katika kufikia malengo” alisema Makala.
 
Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa chuo hicho, Michael Kadinde  alisema  watahakikisha tamasha hilo kongwe nchini  wanafikia vikundi na wasanii  mbalimbali ilikupata kushiriki na kuonesha kazi zao.
 
“Lengo kufikia wasanii wote na hilo tunafanya kila mwaka na zaidi milango ipo wazi kwa mashirika binafsi ya ndani na nje kuja kuwekeza na kukuza sanaa zetu” alisema Kadinde
 
Na kuongeza kuwa kwa sasa TaSUBa ina enzi na kulithisha sanaa na utamaduni kwa vitendo ikiwemo kutoa mafunzo kwa watoto wadogo na wale wa elimu ya msingi.
 
..
Kwa upande wa Vikundi   vinavyoshiriki kwenye tamasha hilo ni pamoja na ;
Alisema, vikundi 40 kati ya 60, ni kutoka Tanzania na vingine ni kutoka nje ya nchi vikiwemo vilivyowahi kushiriki tamasha hilo na vipya ambavyo itakuwa ni mara ya kwanza kuja.
 
Alivitaja vikundi vya Tanzania kuwa ni Ngome International Magic Show – JWTZ,  Splendid Theatre, Kigamboni Community Centre, Malezi Youth Theatre na Jivunie Tanzania Sanaa.
 
Vingine ni Mapoloni Culture Centre, Albino Revolutionary, Cocodo African Music, Imani Theatre, Safi Theatre, Imara Boma, Bagamoyo House of Talents, Bwagamoyo Africulture, Godykaozya & Tongwa Band na Mtoto Mchoraji.
 
Vimo pia Shada Acrobatics, Bagamoyo Players, Bayoice, Jikhoman & Afrika Sana Band, Vitalis Maembe & The Spirit Band na Bagamoyo Dance Company.
 
Aidha, kuna vikundi vya Makini Organization (Arusha), Tumaini Group (Manyara), Kimanzichana Vijana Group (Mkuranga), Utandawazi Theatre Group (Matwi Gha Chalo), kutoka visiwa vya Ukerewe, Hiari ya Moyo (Dodoma), Moshi Police Academy (Moshi), CBM Acrobatic Group, Man Kifimbo Band na Midundo ya Sanaa. Pia kuna vikundi kutoka Ethiopia , Kenya , Norway , Uganda , Rwanda na Ujerumani.

Tuesday, September 24, 2013

Wanafunzi 300 kukosa mikopo

Zaidi ya wanafunzi 300 wa elimu ya juu wa vyuo mbalimbali watakosa mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kutokana na kushindwa kujaza fomu za kuomba mikopo katika kipindi kilichowekwa. 

Watakaokosa mikopo hiyo kwa mwaka wa masomo wa 2013/2014 ni kuanzia mwaka wa pili na kuendelea, ambao hawakujaza fomu za kuonyesha taarifa zao mpya kwa bodi. 
Wanafunzi hao walitakiwa kuwasilisha maombi ya kupewa mikopo kati ya Mei hadi Julai 30, mwaka huu.

Mkugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HELSB, Cosmas Mwaisobwa, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi kuhusu utendaji wa kazi wa bodi hiyo. 

Mwaisobwa alisema kwa kuwa wanafunzi hao hawakujaza fomu za kuomba mikopo, mwaka huu hawatapata fursa hiyo na kwamba kwa mujibu wa utaratibu wao, kila mwaka lazima mwanafunzi aombe. 

Alisema wanafunzi watakaokosa fursa hiyo ya mikopo wameanza masomo yao katika vyuo mbalimbali nchini na kwamba  HESLB haijui sababu zilizowafanya wasiombe. 

Kuhusu ufanisi katika utoaji wa mikopo, Mwaisobwa alisema idadi ya wanafunzi wanaoomba mikopo imeongezeka kutoka 42,729 mwaka 2005/2006 hadi kufikia wanafunzi 97,348 mwaka 2012/2013. 

Aidha, Mwaisobwa alisema bajeti ya kuwakopesha wanafunzi imeongezeka kutoka Sh. bilioni 56.1 mwaka 2005/2006 hadi kufikia Sh. bilioni 306 mwaka 20012/2013. 

Alisema mwaka huu serikali imeitengea bodi hiyo Sh. bilioni 325 kwa ajili ya kuwakopesha wanafunzi wapya, 31,647 na 62,376 wanaondelea na masomo yao katika vyuo mbalimbali. 

Wakati wanafunzi hao wakikosa fursa ya mikopo, mapema mwezi huu, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, aliitaka bodi hiyo kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi na weledi mkubwa kwa mwaka huu wa masomo ili kuepusha migogoro ya wanafunzi kuhusu mikopo.
CHANZO: NIPASHE

Monday, September 16, 2013

Copa Coca Cola yawagusa wanafunzi









Results


Best Goal Keepers - Temeke Girls - Shamimu Hamisi - TZS 500,000/-
                  - (N/A)  Boys  - Beya Yahaya - got TZS 500,000/-

Best Scorers - Mwanza Girls - Yolita Msanyiwa - got TZS 500,000/-
            - Mjini Magharibi Boys - Juma Ally Yusuph - got TZS 500,000/-

Best Players (MVP) - Mwanza Girls - Hamisa Othman (got TZS 500,000/-)
            - Ilala Boys - Ally Mabuyu (got TZS 500,000/-)

Best Referees - Liston Hiari - got TZS 500,000/-

Best Disciplined Team - Dodoma Girls - got TZS 1,000,000/-
                      - Mtwara Boys - got TZS 1,000,000/-

3rd Place - Kinondoni girls - got TZS 2,000,000/-
          - Morogoro boys - got TZS 2,000,000/-

2nd Place - Ilala girls - got TZS 3,000,000/-
          - Ilala boys  - got TZS 3,000,000/-

1st Place - Mwanza Girls - got TZS 8,000,000/-
          - Mjini Magharibi Boys - got TZS 8,000,000/-

Friday, September 13, 2013

Pata tiketi yako hapa ya Dinner ya madawati

Tickets are available at: 

HMT office, Oysterbay Shopping Center
HMT Charity Shop, Kinondoni (near Vijana Hall)
Bianca Salon Spa & Bridal Care, Mbezi Beach (Opp. Ambrosia) 
Amercican Nails TZ, Kinondoni Muslim
Eve Collections, The Arcade Mikocheni
Kiki's Fashion, Oysterbay

Tuesday, September 10, 2013

Mtihani darasa la pili poa-- wazazi


BAADHI ya walimu wa shule za msingi wamefurahishwa na serikali kuanzisha mtihani wataifa wa darasa la pili  kuwa itasaidia kutiliwa mkazo kwa elimu ya awali na kuongeza ufaulu katika mitihani ya darasa la nne.

Aidha,amebainisha kuwa mtihani huo ikiwa utatiiliwa mazona wizara ya elimu ipasavyo tatizo wanafunzi kutojua kusoma au kuandika itakuwa ndoto.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi mkoani Jane Mganwa alisema wamefurahishwa na mpango huo ambao wanaamini utasaidia walimu wa madarasa la kwanza na pili kuongeza juhudi pamoja na wanafunzi wenyewe ili kuepuka kufeli.

Alisema kwani kuna baadhi ya wazazi hawaoni umuhimu wa elimu hiyo na kufanya wanafunzi kuwa mzigo kwa walimu wa darasa la kwanza na pili ambao kwa sasa hawafundishi kusoma na kuandika.

“kwa sasa madarasa hayo mawili wanafundisha masomo saba na siyo uumbaji wa elimu au kusoma hivyo sasa kwa kuwepo mtihani huu watoto watapelekwa shule ya awali”alisema

Naye mwalimu wa Taaluma toka shule ya msingi Vetenary,Amina swai alisema mpango huo utakuwa changamoto kwa wazazi na walimu kutilia mkazo katika kutoa mafunzo na ufuatiliaji ili kuepuka wananfunzi na watoto wao kurudia rudia darasa moja.

Lakini ,Rais wa Chama cha Walimu (CWT)Gratian Mukoba alisema mitihani hiyo ingebakizwa kwa walimu kuchuja kwani kuwepo kutaongeza mzigo kwa wazazi.

Alisema wazazi watakuwa na mizigo ya kulipia mtihani wa darasa la pili,nne,saba,Kidato cha pili na kidato cha nne hivyo walimu wangepewa tamko tu kuwa wasiojua kusoma na kuandika wasivuke darasa la pili.

Juzi ,Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Philipo Mulugo alisema serikali inatarajia kuanziha mtihani mpya wa Taifa kwa wanafunzi wa darasa la pili nchi nzima ili kuchuja watakaoshindwa kusoma,kuandika na kuhesabu.

Alisema mtihani huo ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa matokeo makubwa sasa katika sekta ya elimu kwa lengo la kuondoa uwezekano wa kuwa na wanafunzi katika madarasa ya juu wasiojua kusoma,kuandika na kuhesabu.

Alisema ili kufikia malengo hayo watakaoshindwa mtihani huo watarudia mpaka wajue kusoma na kuandika
Mwisho


Monday, September 9, 2013

Mtihani wa darasa la pili umeanzishwa, nini maoni yako



Na Mwandishi Wetu
MTIHANI mpya wa Taifa, utaanzishwa kwa wanafunzi wa darasa la pili nchi nzima, ili kuchuja watakaoshindwa kusoma, kuandika na kuhesabu.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, alisema hayo jana alipokuwa akitangaza kuanza kwa Mtihani wa wa Taifa wa Kumaliza Elimu ya Msingi Tanzania Bara.

Mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi, unatarajiwa kufanyika kesho na keshokutwa na kuhusisha watahiniwa 868,030 waliosajiliwa.

*Darasa la Pili
Akifafanua uamuzi wa kuanzishwa Mtihani wa Taifa wa Darasa la Pili, Mulugo alisema mtihani huo ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa Matokeo Makubwa Sasa katika sekta ya elimu.

Malengo ya mtihani huo kwa mujibu wa Mulugo ni kuondoa uwezekano wa kuwa na wanafunzi katika madarasa ya juu, wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu na ili kufikia malengo hayo, watakaoshindwa mtihani huo, watarudia mpaka wajue kusoma na kuandika.

Mwaka jana Aprili, Mulugo alipokuwa akizungumza na   wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), alikaririwa akikiri kuwa katika mtihani wa Taifa wa Kumaliza Elimu ya Msingi  wa mwaka juzi, kulikuwa na wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu, waliochaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari.

Kutokana na udanganyifu katika mitihani ya taifa, Mulugo alikaririwa akiagiza wanafunzi wote walioingia kidato cha kwanza wapimwe kwanza uwezo wao wa kusoma na kuandika na kuhesabu.

Alikaririwa akisema tathmini Mkoa wa Kilimanjaro uliongoza kwa kuwa na wanafunzi wengi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu.

"Mkoa wa Kilimanjaro una wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika wapatao 660, Tanga 490 na Dar es Salaam 208," alikaririwa Mulugo bila kutaja matokeo ya mikoa mengine.

“Hili ndilo janga la kitaifa sasa. Siyo hayo mengine ambayo watu wanasema ni majanga ya kitaifa. Lazima tujiulize kwa nini watoto wanamaliza darasa la saba wakiwa hawajui kusoma wala kuandika na halafu wanafaulu?” Alihoji kuongeza:

“Je, siku hizi hakuna tena somo la kusoma na kuandika? Kwa nini mtoto amalize shule bila kuwa na maarifa ya KKK (Kusoma, kuandika na kuhesabu)?  

“Jambo la kusikitisha kuna mpaka baadhi ya wanafunzi wa kidato cha tatu, ambao hawajui kusoma wala kuandika. Tulipofikia siyo pazuri hata kidogo, lazima tuwe makini jamani.

“Tuheshimu Baraza la Taifa Mitihani (Necta), tupate ufumbuzi wa mambo haya taifa hili ni letu sote, lazima tuhakikishe linasimama imara,” alikaririwa Mulugo.

*Darasa la saba
Akitangaza kuanza kwa mtihani wa darasa la saba kesho, Mulugo alisema kati ya watahiniwa wote,  wasichana ni wengi ambao ni 455,925 sawa na asilimia 52.52 ya watahiniwa wote na wavulana ni  412,105 sawa na asilimia 47.47.

Masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii.
Alisema wanafunzi 844,810 wanatarajiwa kufanya mtihani  huokwa lugha ya Kiswahili, kati yao wavulana ni 400,335 na wasichana 444,475.

Wanafunzi 22,535, kati yao wavulana wakiwa 11,430 na wasichana 11,105, wanatarajiwa kufanya mtihani huo kwa lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo walikuwa wakiitumia kujifunzia.

Wanafunzi wasioona waliosajiliwa kufanya mtihani huo ni 88 wakiwemo wavulana 56 na wasichana 32 ambapo pia watahaniwa 597 wenye uoni hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa wanatarajiwa kufanya mtihani huo.

Mulugo alisema maandalizi yote kwa ajili ya mtihani huo yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani, kusambazwa kwa fomu maalum za OMR za kujibia mtihani na nyaraka zote muhimu zinazohusu mtihani huo.

Alitoa mwito kwa maofisa elimu wote wa mikoa na halmashauri kuhakikisha utaratibu wote za mitihani unazingatiwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mazingira yanakuwa salama na tulivu pamoja na kuzuia mianya yote inayoweza kusababisha udanganyifu.

Pia alitoa wito kwa wasimamizi wote kufanya kazi yao  kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu kwa kuwa wapo baadhi ya wasimamizi wamekuwa wakishiriki kuwasaidia watahiniwa kufanya udanganyifu kwenye mitihani yao, na kuonya atakaebainika atachukuliwa hatua kali za kushetria.

 Wanafunzi watakaojihusisha na vitendo vyovyote vya udanganyifu wa mtihani, aliwaonya kuwa atawafutia matokeo yao na kuitaka jamii kutoa ushirikiano unaotakiwa katika kuhakikisha mtihani huo  unafanyika kwa amani na utulivu wa kutosha bila usumbufu wa shughuli za kijamii hasa katika maeneo ya jirani na shule.
Mwisho

Sunday, September 8, 2013

Shule ya wasichana ya Mtakatifu Christina yashinda shindano la Kiingereza



SHULE ya wasichana ya St.Christina imekuwa kinara kati ya sekondari 22 zilizoshiriki
mashindano ya kuzungumza lugha ya Kiingereza ya ‘Bavaria Malt English
Competition for Tanga secondary schools 2013’ yaliyojumuisha wanafunzi zaidi ya
100 kutoka wilaya tano za mkoani humo.

Shule hiyo ilizawadiwa seti moja ya Compyuta na printa ambapo mshindi wa pili
sekondari ya Popatlal iliondoka na seti ya Kompyuta huku Sekondari ya Rosmin
iliyoibuka mshindi wa tatu ikijinyakulia Luninga yenye ukubwa wa inch 40.

Mashindano hayo ya siku mbili yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Regal
Naivera na Mkwakwani kwa  udhamini wa
Bavaria Holland kupitia Kampuni ya Jovet (T) Limited inayosambaza kinywaji
baridi cha Bavaria Malt yalilenga kuhamasisha wanafunzi ili waone umuhimu wa
kuzungumza lugha hiyo.

Akizungumza katika hotuba ya kufunga mashindano hayo na baadae kuwatunuku vyeti na zawadi
washiriki na washindi watatu Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia masuala ya
Elimu mkoani Tanga, Ramadhani Chomola alisema mashindano hayo pamoja na
kuwawezesha wanafunzi kutambua uwezo wao pia yamewapa mwamko mpya wa kuzungumza
lugha hiyo.

“Nazipongeza shule na wanafunzi wote walioshiriki mashindano ya mwaka huu wito wangu
nawataka waongeze ubunifu na bidii ya kuzungumza Kiingereza popote wanapokuwa
ili waweze kujijenga na kwa wale walioshinda leo wasijiamini sana na kuridhika
bali wachukulie mafanikio hayo kama hatua ya kuendeleza harakati za kuwasiliana
kwa kutumia lugha hiyo ya kimataifa”,alisema.

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo Meneja wa Uendelezaji Masoko wa BavariaHolland, Roger
ter Horst alisema kampuni hiyo inaamini kwamba ni jambo jema kusaidia jamii
kufikia malengo yake ya kupata maendeleo yake ya kiuchum na kijamii.

“Mashindano haya tumeyaasisi kwa mara ya kwanza hapa Tanga ili kurudisha shukrani kwa jamii
inayotumia bidhaa zetu tumeanza kwa kuangalia hawa vijana walioko shuleni kwa
kuwapa fursa hii ya mashindano inayowawezesha kujipa muda zaidi wa kuzungumza
Kiingereza ambayo ni miongoni mwa lugha muhimu inayotumika kwenye masomo yao na
kuwasiliana ki kimataifa”, alisema.

Nao baadhi ya wanafunzi walioshiriki wakiwemo Radhia Abubakar wa St. Christina na Sammy
Madundo wa
Popatlal aliyejinyakulia zawadi ya kompyuta ndogo (Laptop) kutokana na umahiri
na juhudi binafsi aliyoonesha kwenye mashindano hayo alisema yamempa changamoto
inayomsukuma kuongeza juhudi katika kujifunza lugha hiyo.

“Kiukweli lugha ya kiingereza sio rahisi kamlugha nyingine hii inamhitaji mtu kujifunza kwa bidii na kuizungumza wakati
wote ndipo ataweza kuwa na misamiati mingi ya kumwezesha kuitumia kwa ufasaha
binafsi pamoja na wenzangu wanne tuliowakilisha shule yetu ilitugharimu muda
mwingi wa ziada kujifunza mambo mbalimbali yaliyomo kwenye lugha hii”, alisema
Radhia.

Mashindanohayo yanatarajiwa kuendelea mwakani kwa kujumuisha sekondari nyingi zaidi
kutoka katika wilaya zote nane zenye halmashauri 11 zinazounda mkoa wa Tanga.


Thursday, September 5, 2013

Tukio hili ni muhimu kwetu wadau wa elimu hivyo twendeni tukasaidie


Monday, September 2, 2013

Onesho la elimu la Elimu Expo limefungwa rasmi, lilifana sana

Wanafunzi wa shule ya Premier Girls Secondary School wakionesha uwezo wao katika somo la Kemia


Hawa ni wanafunzi wa Secondary ya Loyola

wamebuni namna ya kutengeneza progamu mbalimbali za kompyuta

wakiwa kazini

Wachapishaji na wasambazaji wa vitabu kutoka kampuni ya Aidan



Hapa wataalamu kutoka Aida wakitoa maelezo kwa mgeni aliyetembelea banda lao

Wafanyakazi wakiangalia kitu katika kitabu




Wanafunzi wa shule ya msingi ya Uhuru Mchanganyiko wakiwa katika banda lao wakiimba pamoja huku mwenzao akipia gitaa wakati wa maonesho ya Elimu Expo yaliyomalizika juzi (Picha na Evance Ng'ingo

Msanii Lulu sasa kurudi shule, uzinduzi wake wafana

Wasanii wakongwe waliohudhuria uzinduzi huo

Steve

Jb na wazungu wanaotengeneza siri ya mtungi

Lulu na meneja wake Rukaza

Yahaya, Dude

Msanii Lulu akiimba

Mama Kanumba akipewa mihela na Wema

Wageni
Habari
Msanii wa filamu Elizabeth Michael ambae amezindua filamu yake jusi ya Foolish Age amesema kuwa kwa sasa mpango wake pi ani kurudi shule kuongeza elimu.

Aliiambi abolg hii kuwa amekuwa akifanya sanaa kwa muda na kwa sasa anaona kuwa ngoja asomee masomo mengine mbali na kuwa ataendelea kufanya sanaa yake kama kawaida