Help Children
Love them
Saidia Watoto

Monday, August 27, 2012

Wasanii watakiwa kuijendeleza kitaaluma

Mkufunzi wa masuala ya aundaaji wa Filamu kutoka taasisis ya Sanaa na uandishi wa Habari (IAMCO) Ngalimecha Ngahyoma, akizungumza jambo katika Jukwaa la Sanaa, kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) Hassan Bumbuli na kushoto ni Katibu Mtendaji wa

Friday, August 24, 2012

Isome hii ni muhimu kwa wadau wa elimu ya juu


TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UENDESHWAJI WA UDAHILI - ELIMU YA JUU KWA MWAKA WA MASOMO 2012/2013 UTANGULIZI Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (‘Tanzania Commission for Universities’-TCU) ikishirikiana na B 
araza laTaifa la Elimu ya Ufundi (‘National Council for Technical Education’ - NACTE) pamoja na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi Elimu ya Juu (Higher Education Students Loans Board) inapenda kuutarifu umma kuhusu utaratibu wa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2012/2013 kupitia mifumo ya “Pre-entry”, “Mature Age Entry”, “Equivalent Qualifications” na mfumo wa pamoja wa udahili (‘Central Admission System’) na utaratibu wa mikopo kama ifuatavyo: 1. MFUMO WA UDAHILI KUANZIA MWAKA 2012/13 1.1 Utaratibu wa Kuendesha Program za “Pre-entry”

Wednesday, August 22, 2012

UMOJA WA WANAFUNZI WATANZANIA WANAOSOMA KENYA WACHANGIA KAMPENI YA UJENZI WA HOSTELI ZA WASICHANA


Meneja habari wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Sylvia Lupembe Gunze akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya kampeni ya ujenzi wa hosteli za wasichana.Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania Bi. Rosemary Lulabuka akifuatiwa na Mwenyekiti wa Wanafunzi wanaosoma nchini Kenya katika chuo cha United States International University (USiU) waliofika kutoa mchango wao katika ofisi za Mamlaka ya Elimu Tanzania.

Monday, August 20, 2012

Zantel yasherehekea sikukuu ya Iddi na watoto wa kituo cha watoto yatima, pia yawapatia vifaa vya kujifunzia

Watoto wa kituo cha Al-Husein cha Magomeni wakicheza pamoja na mchekeshaji huyu wakati wa sherehe ya idi pili iliyoandaliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Zantel ikiwa ni ishara ya upendo kwa watoto hao. Tukio hilo lilifanyika katika ofisi za Zantel zilizopo drive inn.

Tuesday, August 14, 2012

Jarida la Manispaa ya Ilala lazinduliwa rasmi, linaelimisha na kutoa taarifa mbalimbali za Ilala

Meya wa Ilala azindua jarida maalum lenye kubeba ujumbe wa manispaa hiyo kuhusiana na elimu na masuala mengine ya maendeleo Pichani Meneja wa masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Linda Chiza akikabidhiwa jarida la Ialala na Meya wa Manispaa hiyo ikiwa ni inshara ya kutambua mchango wa benki hiyo katika kufanikisha uchapishwaji wa jarida hili

Sunday, August 12, 2012

Chuo Kikuu Dodoma chamwagiwa misaada ya vitabu 300 kutoka Tigo

\ makamu mkuu wa chuo cha UDOM, profesa Ludovick Kinabo (katikati) akiishukuru kampuni ya Tigo kwa kuendelea kuchangia maendeleo ya chuo cha UDOM, pembeni yake ni meneja uhusiano na udhamini wa Tigo Bw. Edward Shila pamoja na mkurugenzi wa Tigo kanda ya kati, Fadhila Said.

Wednesday, August 8, 2012

Mabalozi wa kuchangia ujenzi wa mabweni wavamia bungeni

Mh. Sophia Simba Waziri wa maendeleo ya jamii jinsia na Watoto akitoa mchango wake kuchangia kampeni hii bungeni. Ili kuchangia pia unaweza kutuma neno CHANGIA TOFALI kwenda namba 15564 ambapo utakatwa shilingi 250 tu za kitanzania.

Tuesday, August 7, 2012

Tujiunge katika Dar Fashion Festival


Saturday, August 4, 2012

Mwasiti na Banana watoa elimu ya muziki kwa washiriki wa Epiq BSS 2012

Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la Tanzania House of Talent (THT) Mwasiti Almasi akiwafundisha washiriki wa shindano la Epiq Bongo Star Search (EBSS 2012) kuimba baadhi ya nyimbo shindano hilo litaanza kurushwa rasmi leo na limedhaminiwa na Zantel

Thursday, August 2, 2012

Maelfu wanufaika na elimu ya muziki kutoka EBSS Coco beach

Umati mkubwa wa watu waliojitokeza katika usaili wa shindano la kuinua vipaji la epiq bongo star search (ebss) katika fukwe ya coco
Majaji wa shindano la epiq bongo star search wakionekana kufurahishwa na moja kati ya vipaji vilivyojitokeza jana katika usaili unaomalizika leo coco beach
Kijana huyu aliamua kutumia kinanda ili kuwavutia majaji katika usaili wa shindano la epiq bongo star search (ebss)

Wednesday, August 1, 2012

JOOMLA! CMS WEBSITE DESIGN AND DEVELOPMENT TRAINING FROM 3RD SEPTEMBER, 2012 - 7TH SEPTEMBER, 2012

The University of Dar es Salaam (UDSM), College of ICT (CoICT) is organizing a 5 days training to equip participants with the skills, knowledge and techniques of developing and maintaining good websites without even being experts by using Open source Content Management System (CMS) called Joomla! CMS 2.5.6 Joomla is an award-winning CMS, which enables people to build Websites and it has powerful online applications. A summary of course outline can be found from the College website: www.coict.udsm.ac.tz Target Audience • Individuals who would like to have their very own website. • Owner of an existing Joomla website built by another 3rd party. • SMEs and small businesses who wish to cut down the costs of web development projects and manage their own websites. • Individuals who wish to be self-employed in Website development • Web masters, website administrator, computer systems analysts, public relationship officers, communication officers and entrepreneurs. Training fee: Tsh. 600,000/= (excluding breakfast and lunch) Venue: UDSM Kijitonyama Campus (Former TTCL Staff College) , Dar Es Salaam Registration: Please register NOW through the College website: www.coict.udsm.ac.tz For more information contact us at mtebe@udsm.ac.tz; Telephone: +255715383366

MABALOZI WA HARAMBEE YA UJENZI WA HOSTELI ZA WASICHANA WA SEKONDARI WAZINDUA KAMPENI YA “ELIMU YAO, WAJIBU WETU”



Kikundi cha wasichana maarufu watano katika nyanja mbalimbali nchini wameungana kwa pamoja na kuamua kwa hiari kuunga mkono jitihada za Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) za kutafuta kiasi cha shilingi za kitanzania billion 2.3 zitakazotumika kujenga hosteli 30 ambazo zitahudumia wasichana wa shule za sekondari 1,504. Kikundi hicho cha mabalozi wa kampeni hii kinaundwa na Rebeca Gyumi(Mtangazaji wa kipindi cha FEMA) Faraja Nyalandu (Miss Tanzania 2004), Nancy Sumari (Miss Tanzania 2005) Jokate Mwegelo(Mshindi wa pili Miss Tanzania 2006) na Mariam Ndaba(Mwana mitindo na mmiliki wa blog) kiliguswa kwa namna ya kipekee na na jitihada za TEA na hivyo wakaamua kwa hiari kuungana na TEA katika kuhamasisha watu kujitokeza na kuchangia kampeni hii. Lengo la Mabalozi hawa ni kuhamasisha uchangiaji na kuwezesha kujenga zaidi ya hosteli 5 kati ya 30 ambazo TEA imepanga kujenga. Katika Uzinduzi huo uliofanyika Tarehe 31/07/2012 katika hoteli ya Serena Jijini DSM kati ya mabalozi hao na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ambapo ni Faraja Nyarandu pekee ndie alikosekana kutokana na kubanwa na majukumu mengine lakini alithibitisha uwepo wake katika kampeni zinazoendelea