Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, July 2, 2013

Chuo cha Afya kipya kujengwa mwezi ujao


CHUO Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili(MUHAS)  kinaanza mwezi ujao kujenga chuo kipya kwa ajili ya mazoezi katika eneo la Mloganzila, Kibamba jijini Dar es  Salaam.

Ujenzi huo  unatarajiwa kuanza Agosti mwaka huu katika eneo hilo na kikimalizika, kitachukua wanafunzi 15,000 watakaosoma  taaluma  mbalimbali za afya.

Akizungumza  na waandishi wa habari  jana kwenye   Maonesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa  yanayoendelea katika viwanja  vya  Mwalimu  J. K Nyerere  jijini  Dares Salaam (sabasaba) ,Ofisa Mipango Mkuu wa chuo hicho Ulimbaga Kijobile alisema  ujenzi wa  chuo hicho, unakadiriwa kufanyika ndani ya mwaka mmoja na wanafunzi wa muhula wa kwanza wanatarajiwa kuanza chuoni hapo mwaka 2015.


Kijobile alisema  uamuzi  huo umetokana na  ongezeko la wanafunzi hivyo kuwa wengi.
Alisema  eneo hilo   litawezesha wanafunzi hao kupata sehemu  za kusomea kwa ufanisi  kama vile  maabara za kisasa, madarasa, na sehemu za kufanyia mazoezi.


“Tumeamua kuanzisha mradi kwa kujenga chuo kipya kwa sababu MUHAS ina sehemu ndogo na hatuwezi kuipanua kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa chuo ili kuweza kutosha kwa wanafunzi” alisema Kajobile.


Aidha alisema wanafunzi hao , walikuwa wakipata tabu katika kufanya mazoezi ,hivyo hulazimika  kwenda  hospitali za Mwananyamala na Amana.


“Muda mwingine tunatumia hospitali nyingine ili kupata sehemu ya kutosha lakini hospitali hii itakayojengwa itasaidia kuchukua wanafunzi wote ili kuweza kufanya mazoezi yao bila usumbufu” alisisitiza Ulimbaga.


Alisema  ujenzi wa  chuo hicho, unakadiriwa kufanyika ndani ya mwaka mmoja,ambapo  wanafunzi wa muhula wa kwanza wa mwaka 2015 wanatarajiwa kuanza.


Aliongeza  kuwa kitatoa huduma za kiafya kama hospitali nyingine hivyo baada ya ufunguzi wake, wananchi watapata matibabu chuoni hapo

0 comments:

Post a Comment