Help Children
Love them
Saidia Watoto

Thursday, July 25, 2013

Elimu ya bongo inapoteza wenye ujuzi-- IUCEA

BARAZA la Elimu la Vyuo Vikuu vya Afrika  Mashariki (IUCEA) limesema  mfumo wa elimu nchini umekuwa ukipoteza watu wenye ujuzi wa mambo mbalimbali  kwa kigezo cha kushindwa katika mitihani ya kumaliza masomo.

Katibu Mtendaji wa wa baraza hilo, Profesa Mayunga Nkunya alisema wanafunzi wasihukumiwe kwa kushindwa mtihani bali aangaliwe upande mwingine, ni nini anaweza kufanya kuinua uchumi.

“Utaratibu wa sasa wa elimu unakotupeleka hakufai kabisa…kigezo cha kuangalia kufaulu ama kufeli tu kwa mwanafunzi sio suala jema kwani wapo wengi wanaokuwa wavumbuzi na wenye ujuzi mbalimbali ambao hawapewi nafasi,” alisema Profesa Nkunya na kutaja, Rwanda kwamba  wanaotekeleza mfumo unaompandisha mtu alipo bila kuangalia mtihani.

Profesa  Nkunya alisema hayo Dar es Salaam wakati akizungumzia ushirikiano uliopo kati yao na Baraza la Biashara la Afrika Mashariki (EABC) katika kupambana na  ukosefu wa ajira kwa vijana.

Mabaraza hayo yameandaa mkutano wa Afrika Mashariki wenye kujadili mahitaji ya soko la ajira kwa kuzingatia taaluma. Mkutano huo utafanyika Oktoba 24 na 26 jijini Nairobi, Kenya.

Alisema Baraza hilo litatayarisha mkakati wenye kujikita zaidi katika kuangalia ujuzi kwenye taaluma kama ilivyo Rwanda ambao utahakikisha suala la elimu linaendana na ajira katika nchi hizo.


0 comments:

Post a Comment