Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, June 23, 2013

Fast Jet ilivyonogesha Siku ya Muziki Duniani, mengi ya kujifunza

Fast Jet's Commercial Manager Jean Uku

Wafanyakazi wa Fast Jet

Wakitoka kumpongeza msanii ambae ni mfanyakazi wa Fast Jet Nyemo




IKIWA juzi ilikuwa ni siku ya muziki duniani wasanii  mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya juzi walitoa burudani safi katika onesho la siku ya Muziki Duniani lililofanyika  katika viwanja vya Posta, Kijitonyama.

Tukio hilo lililodhaminiwa na kampuni ya ndege ya Fast Jet iliwashirikisha wasanii Elias Barnaba, Godzila, Kala Jeremiah na wasanii wengine mbalimbali wa utamaduni.

Huku lengo lake ni kuwakutanisha wadau wa muziki pamoja na wasanii ikiwa pia na lengo la kuwa na mwelekeo mpya wa sanaa na muziki.

Pia katika kuongeza hamasa mfanyakazi wa kampuni ya Fast Jet Nyemo Mwiluka aliimba wimbo wake wa Njoo Turuke na Fast Jet.

Pia aliimba nyimbo zake nyingine mbalimbali huku akisindikizwa na madansa wake pamoja na wasanii wengine.

Tamasha hilo lilidhaminiwa na Fast jet, Alliance France, Goethe Institute na Pepsi ambapo hufanyika kila mwaka Juni 22.
Akizungumzia udhamini wake wa tukio hilo Meneja Biashara wa Fast Jet Jean Uku alisema kuwa kampuni hiyo mbali na kutoa huduma usafiri pia imeamua kusaidia masuala ya sanaa kwa kuwa inatambua nafasi ya sanaa katika kukuza ajira hususan kwa vijana.
Ends

0 comments:

Post a Comment