Help Children
Love them
Saidia Watoto

Thursday, December 6, 2012

Shule ya Chekechea yafungwa kwa muda





UJENGAJI wa fremu za maduka 10 mbele ya shule ni kinyume cha sheria hivyo NAIBU Waziri wa elimu na Mafunzo ya Ufundi,Philipo Mulugo moja kati ya shule aliyoifunga ni ya Mwenyekiti wa SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) mkoa wa Dar es salaam , Hassan Kaumo kwa Aidha,Waziri amehaidi kufuatilia usajili wa shule hiyo kwani inaonekana kusajiliwa mwezi June kwa madai maduka hayo hayakuwepo wakati mwezi Septemba Naibu waziri aliobaini kuwapi kwa maduka katika shule.

Shule hiyo ya Awali na Msingi ya Heroes iliyoko Chanika wilaya ya Ilala imefungiwa hadi itakapobomoa maduka hayo hao kuihamishia sehemu nyingine.
Akiwa katika ziara ya kutembelea shule ,Mulugo alifika shuleni hapo na kufunga shule hiyo na kumtaka mmiliki kufikia mwezi Januari asipokee  wanafunzi mpaka warudishe majengo kama ilivyosajiliwa.

“ninafunga matumizi ya shule ya elimu ya awali na msingi mpaka afike wizarani na wakaguzi waone amefanya marekebisho au kuhamia sehemu nyingine kwani amechanganya biashata za  maduka na shule “Alisema
Mmiliki wa shule hiyo,Kaumo alikubali kufanya makosa ya kujenga maduka na kuhaidi kufanya marekebisho kwa kubomoa maduka wiki ijayo nakurudisha kama ilivyokuwa mfumo wa zamani.

Anasema Lengo lilikuwa kuwa na biashara zinazoendana na mahitaji ya wanafunzi shuleni hapo,na alipopata taarifa ya Naibu waziri kupita na kukemea maduka shuleni aliyafunga yote.

Katika Shule ya Deli iliyopo Pugu ,alibaini shule hiyo kutosajiliwa lakini ikiendelea kutangazwa kutoa elimu ya kitaifa ya shule ya awali na uangalizi maalum wa watoto.
alipofika shuleni hapo alikuta wakiendelea kuandika tangazo mlangoni na kuamlishwa kulifuta kwani haijasajiliwa kutokana na eneo lake kuwa dogo huku likizungukwa na maduka.

Aliyekuwa Mwalimu wa taaluma shuleni hapo,Talile Hussein  alikiri kutosajiliwa na kwamba awali ilikuwa sekondari lakini baada ya kupata matatizo ya kidato cha pili mwaka jana waliwataka wazazi kuhamisha wanafunzi wote na kubaki kituo cha twisheni.
Alisema sasa wako katika mpango wa kuanzisha shule ya kimataifa ya awali na wamenza kutangaza bila kusajili na katika eneo hilo ambalo awali walikataliwa kusajiliwa kutokana na kuwa dogo.
Mwisho


0 comments:

Post a Comment