Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, December 23, 2012

Mmiliki wa Hoteli ya Peacock Mfugale atoa somo kwa wafanyabiashara ndogondogo

Mfugale akimkabidhi mwakilikishi wa TBC 1 zawadi kwa kuonesha inshara ya shukrani kutokana na msaada wa Redio hiyo katika kukuza biashara zake

Mmiliki wa hoteli hiyo Mfugale akitoa neno la shukrani kwa waandishi kuwashukuru kwa msaada wao katika kusaidia kukuza biashara zake za hoteli

Mwandishi wa Chanel Ten Kibwana Dachi akitoa neno la shukrani kwa niaba ya waandishi waliohudhuria

Waandishi walipata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali siku hiyo kabla ya kuanza ziara ya kutembelea vyumba vya hoteli yake mpya

Hiki ni chumba chenye hadhi ya kidiplomasia

Mfugale aliongozana na waandishi hadi vyumbani ambapo alipata fursa ya kuwafafanulia masuala mbalimbali

Sehemu za ndani za vyumba hivyo

Mahala pa kunawa mikono

Hapa akiwaonesha jakuzi lililopo katika moja ya vyumba vya hoteli hiyo

Ulifika wakati wa kusakata muziki ambapo wafanyakazi na waandishi kwa pamoja walicheza

Wafanyakazi wa East Africa Television wakiwa na Mfugale

Habari Kamili


MMILIKI wa hoteli za Peacock nchini Joseph Mfugale ametoa elimu kwa wajasiriamali wanaochipukia kuepuka kukata tamaa na badala yake wajikite zaidi katika kujiendeleza kielimu na kibiashara kiujumla.

Alisema hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maadhimisho ya miaka 20 tangia kuanzishwa kwa hoteli yake ya Peacock iliyopo Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

Akizungumzia mikakati ya maendeleo ya hoteli zake Mfugale alisema kuwa kwa sasa anampango wa kujenga hoteli ya nyota tano katika eneo la Kigamboni itakayokuwa na uwanja wa gofu humohumo.

Mfugale alisema hayo juzi wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika hafla fupi ya kusherehekea miaka 20 tangia kuanzishwa kwa hoteli ya Peacock iliyopo Mnazi Mmoja, Dar es salaam.

Mfugale alisema kuwa kwa sasa biashara ya hoteli inazidi kukua kwa kasi hapa nchini na kuna kila sababu kwa wawekezaji wazawa kuhakikisha kuwa wanawekeza katika sekta hiyo iliyoajili watu wengi.

Alisema kuwa kwa kipindi cha miaka 20 tangia kuanzishwa kwa hoteli ya Peacock  ya Mnazi Mmoja tayari amepanua biashara za hoteli kwa kujenga jengo jipya la hoteli hiyo lililopo nyuma  ya hoteli hiyo lenye vyumba.

Alisema kuwa pia anaendelea na ujenzi wa jengo la Peacock lililopo Iringa mjini ambalo lotaisaidia kuongeza ajira kwa vijana katika mkoa huo pamoja na kuwahifashi watalii.

Waandishi wa habari walipata fursa ya kutembelea vyumba vya jengo jipya la Peacock la Mnazi Mmoja ambapo kuna vyumba vya hadhi ya raisi, wanadiplomasia pamoja na watu wa kawaida.
Mwisho.


0 comments:

Post a Comment