Help Children
Love them
Saidia Watoto

Thursday, November 1, 2012

UDOM yamwagiwa vifaa vya michezo na LAPF


Na Katuma Masamba
MFUKO wa Pensheni wa Watumishi wa  Serikali za mitaa (LAPF) jana  umetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya michezo vyenye thamani ya Sh milioni 8.5 kwa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Akikabidhi msaada huo Meneja wa LAPF kanda ya Mashariki Lulyalya Sayi alisema, wanatambua umuhimu wa michezo nchini na hasa katika kujenga  kiafya za wananchi na ndio sababu kubwa iliyovuta  kutoa vifaa hivyo ikiwa ni seemu ya majukumu ya mfuko huo kuhudumia jamii ya Watanzania.

Alisema licha ya kuwa na mahitaji makubwa, wameona ni vyema kutoa kile walichoweza wakiamini kwamba itasaidia kufanikisha michezo ya mwaka huu ya Jumuiya ya michezo ya vyuo vikuu nchini (TUSA) kwa kuwa utakidhi mahitaji muhimu hasa jezi na mipira.

“Ni muhimu kuendeleza michezo kwani huleta nguvu na afya, na LAPF inawaomba msisite kuendelea kuwasilisha maombi ya vifaa kama hivi vya michezo au vingine na sisi tutasaidia kila tutakapoweza” alisema Sayi.

Aidha, aliongeza kuwa LAPF imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia kuendeleza michezo nchini ambapo kwa mwaka jana walitoa vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na vifaa vya michezo kwa jumuiya ya michezo ya vyuo vikuu nchini (TUSA) kwa ajili ya michezo kitaifa.

Naye Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala   Profesa Shabani Mlacha ameishukuru LAPF kwa  msaada huo ambao amesema utasaidia katika kuendeleza michezo chuoni hapo na kuendeleza vipaji vya wanafunzi.

Msaada uliotolewa ni pamoja na jezi jozi 27, 10  kwa ajili ya netiboli na 17 kwa ajili ya mpira wa miguu, mipira 25, vizibao jozi 24, soksi, glovu seti mbili pamoja  na nyavu  nne za mpira wa wavu  .
MWISHO.

0 comments:

Post a Comment