Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, April 14, 2013

Mjadala wa mustakabali wa Elimu ulivyojiri UDSM

Wadau wengi wa elimu walijitokeza

Wahadhiri pia walikuwapo

Watoa mada

Mbati hakukosekana  
Habari kutoka gazeti la HabariLeo
MDAHALO wa kitaifa wa elimu uliofanyika jana umebainisha kiini cha kuporomoka kwa kiwango cha elimu nchini ambacho ni walimu, viongozi wa serikali, wananchi na wazazi kwa ujumla.

Akichokoza mada kwenye mdahalo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitila Mkumbo alisema utafiti walioufanya unaonyesha kuwa shule zinazofundishwa walimu wenye sifa ndizo ambazo hazifanyi vizuri kuliko zile zinazofundishwa na walimu wenye stashahada na wanaofundisha kwa kuwa na leseni pekee.

Alisema kuwa katika utafiti huo waliuliza maswali mawili ya kwanini wamechangua kusomea fani ya uwalimu na je wanampaka wa kukaa kwa muda gani kwenye taaruma na majibu hayo yaonyesha wale wenye elimu ya stashahada walikuwa na uhakika wa kuendelea kufundisha kuliko wale wenye shahada.

 “Shule ya Mukoba (mwenyekiti wa CWT-Gracian) ni miongoni mwa shule zenye walimu wengi wenye sifa, lakini inawanafunzi wengi wenye divisheni 0, lakini shule kama Maria inawanafunzi wenye stashahada wanafany vizuri.

Mkumbo aliongeza: “Ningekuwa ni Waziri wa Elimu ningeajiri walimu wenye diploma (stashahada) na kuachana na wenye shahada maana hawa hawatulii na wengi wao walipojiwa walisema kama ukimaliza kutohoji ikatokea kazi naondoka sasa hivyi.”

Mkumbo alisema pia udogo wa mishahara kwenye shule za umma ndizo zinazowafanya walimu wengi kutotulia shuleni kuliko wale wanaofundisha katika shule za watu binafsi na mashirika ya dini.
“Katika wagonjwa elimu wa Afrika, sisi tunakaribia kutoka wodini kwasababu tumefanikiwa katika kuingiza watoto wengi shule ya msingi, sekondari na katika vyuoni.

 Ni lazima tuwekeze sana kwenye elimu kwasababu ni taifa la watoto kwani asilimia kubwa ya vijana. Hata tukijivunia kuwa tuna gesi tukiwa hatuna akili gesi itatulipukia,” alisema.

Aidha alisema kunahatari kubwa ya mwaka 2015 kwa vyuo binafsi kukosa wanafunzi kufuatia matokoe ya kidato cha nne ya mwaka jana na kushauri kuwa wale waliopata daraja la tatu bila kuwa na alama nzuri wapewe mafunzo maalumu na wale wa kidato cha nne wafundishwe na kurudia mtihani na wale waliopata daraja sifuri warudie kwa nguvu zao wenyewe.

Naye mtaalamu wa mipango ya elimu na utawala, kubuni program na tathimini profesa Herme Mosha alisema mfumo wa kuwachagua wanafunzi wanaokwenda kusomewa uwalimu wakiwa ni wale wasiofanya vizuri kwenye mitihani yao kwani watu hao wanakuwa na upungufu wa maarifa kwa asilimia 70 hivyo vigumu katika kuwafanya watoe wanafunzi wenye alama A.


Mkumbo alisema kunahaja ya kuweka suala la elimu kuwa kipaumbele cha taifa na na kuwekeza katika elimu huku akinukuu viongozi mbalimbali akiwamo Hayati Mwalimu Julius Nyerere, na Waziri Mkuu wa Uongereza Tony Blaia waliozungumza na kutilia mkazo suala la elimu huku Rais Benjamini Mkapa kipaumbele chake kuwa ni uchumi.

Akimnukuu nyerere “ atuna jaha ya kutozungumzia elimu na mataifa makubwa yataumia elimu kama nyenzo kuu ya kutugandamiza.”
Akinukuu Blair alisema “ukiniuliza tena kipaumbele katika sera yangu ni elimu, elimu elimu wakati Rais mstaafu Benjamini Mkapa alisema kipaumbele change ni uchumi, uchumi, uchumi.

Akitoa mada ya usawa, fulsa na ubora wa elimu Profesa Adolf Mkenda alisema viongozi wengi hawaweki kipaumbele katika elimu 

“ Wanaopigia kelele sera na kuzisimamia watoto wao hawasomi kwenye shule hizo, wenzetu Uingereza Tony Blair walimuhoji ni kwanini watoto wake hawasomi shule za umma lakini je hapa tunaweza kuhoji?

Mkenda alioongeza: “Mtu anayesimamia kitu ambayo hakimuusu moja kwa moja je anaweza kuwa na nafasi ya kufanya vizuri?”

Hata hivyo, kuwa kuna haja ya walimu kuongezewa mishahara kuliko ilivyo sasa kwani hali hiyo inachangia kuzorotesha mori wa kufundisha.

Akitolea mfano, Mkumbo alisema walimu waliomaliza shahada ya uwalimu kwa miaka mitatu huwanza na mshahara mdogo ukilinganisha na taaluma zingine  na pia kushauri kuwapo kwa shule maalumu za kitaifa ambazo zitasimamiwa na wizara na kuwa shule za kata zibaki mikononi mwa halimashauri


Haidham watu mbalimbali waliochangia madahalo huo wametaka kuwapo ushirikiano kati ya walimu na wazazi katika suala zima la elimu kwa mwanafunzi na kuonya kuacha kuwa buzy kutafuta ada bila kujua elimu wanayopata watoto zao.

0 comments:

Post a Comment