Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, March 24, 2013

Mwalimu aingia mkutanoni akiwa na nguo za kike


KATIKA hali ya kushangaza, mwalimu wa kiume katika shule ya msingi Chididimo Kata ya Zuzu katika Manispaa ya Dodoma (jina tunalo),  juzi alitinga mkutanoni akiwa amevalia sketi na blauzi ya kitenge huku akiwa amesuka nywele za bandia na kuzua gumzo mkutanoni hapo.

Licha ya mwalimu huyo kuvaa viatu vya kiume na soksi fupi, alikuwa akitembea mwendo wa kiume huku mikanda ya sidiria aliyokuwa ameivaa kujitokeza mara kwa mara.

Haya yalitokea katika kijiji cha Chididimo wakati wa Wiki ya Maji kimkoa, ambapo pamoja na mambo mengine kulikuwa na uzinduzi wa mradi wa maji.

Mwalimu huyo alikuwa kati ya wacheza ngoma wa kikundi cha Mpango Kazi Chididimo, lakini ilikuwa ni vigumu watu wasiomfahamu kumtambua. Hata hivyo watu walianza kupata wasiwasi kuwa hakuwa mwanamke wakati kikundi hicho kilipoingia uwanjani, ambapo alikuwa akiimba kwa sauti nzito.

Lakini, maswali ya wageni waliohudhuria mkutano huo, yalipata majibu mara baada ya mwalimu huyo kupanda jukwaani akiwa na mwenzake kwa ajili ya kuimba shairi.
Kutokana na hilo ndipo wanakijiji walipoanza kutoa siri kuwa alikuwa ni mwanaume na ni mwalimu wa shule ya msingi kijijini hapo.

Kutokana na utata na minong’ono iliyosambaa mkutanoni hapo,  mwongozaji wa sherehe hizo alimfuata mwalimu huyo na kuzungumza naye kwa muda na aliporudi alikuwa tayari na jina la mwalimu huyo na kusema kuwa mwenye nywele ndefu ameshalifahamu jina lake kisha kulitaja.

Mshereheshaji huyo alisema hata  nyimbo na shairi ambalo wanafunzi waliimba, alitunga mwalimu huyo ambaye ni mahiri katika sanaa.
Mwalimu huyo alikiri kuwa sanaa ipo kwenye damu yake na alifanya hivyo kama msanii.

0 comments:

Post a Comment