Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, March 19, 2013

Wanawake saba wapanda Mlima Kilimanjaro na kutembelea shule mbalimbali hapa nchini

Huyu ni mmoja kati ya wanawake waliopanda Mlima Kilimanjaro yeye ni Mtanzania
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Utalii ya nchini Nepal  Subash Niroula akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa Utalii wa Wizara ya Maliasili na Utalii Ibrahim Mussa wakati wa hafla ya kuwaaga wanawake saba kutoka nchini Nepal waliopanda Mlima Kilimanjaro katioka maadhimisho ya siku ya wanawake duniani
Mkurugenzi wa Utalii wa Wizara ya Maliasili na Utalii Ibrahim Mussa akizungumza katika hafla hiyo
                       
Picha ya pamoja na wanawake waliopanda mlima huo

Musa na mkewe huyo wa katikati

Mimi pia nilipiga picha na wanawake hao

                                                              
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Aloyce Nzuki na Mkurugenzi wa Utalii wa Wizara ya Maliasili na Utalii Ibrahim Mussa wakiwa katika picha ya pamoja katikati ni Mrs Mussa  



KIONGOZI wa kundi la Wanawake Saba kutoka nchini Nepal waliopanda mlima Kilimanjaro, Shailee Basnet, ameitaka serikali pamoja na wanajamii kusaidia kupambana na manyanyaso dhidi ya wanawake nchini.

Alisema kuwa katika kusaidia kampeni dhidi ya manyanyaso ya wanawake duniani wamekuwa na utamaduni wa kupanda milima mirefu duniani na kufikisha ujumbe wa kutetea haki za wanawake ambapo wameshapanda milima Everest na Mlima Kilimanjaro.

Alisema kuwa wakiwa hapa nchini wametembelea shule mbalimbali kutoa elimu ya kujiamini na kujitambua kwa wanafunzi wa shule mbalimbali.
 
Wakati huohuo Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Utalii ya nchini Nepal Subash Niroula alisema kuwa tayari wamenza kukutana na wamiliki wa kampuni za Utalii za hapa nchini.

Niroula alisema kuwa Tanzania kuna vivutio vingi vya utalii ambavyo vinatakiwa kutangazwa nchini Nepal na sehemu nyingine duniani.

Alisema kuwa ili kufanikisha utangazwaji wa utalii huo kunahitajika kuwepo kwa juhudi binafsi kutoka kwa wadau wa utalii wa Nepal na Tanzania kushirikiana pamoja ili kufanikisha ukuaji wa utalii huo.

Alisema kuwa Mlima Kilimanjaro unafahamika zaidi nchini Nepal na unaweza kutangazwa kikamilifu zaidi ili kuongeza idadi ya watalii wanafika Tanzania.


Mwisho



0 comments:

Post a Comment