Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, March 24, 2013

Shule ya wasichana ya Henry Gogarty yatembelewa na Lowassa


WAZIRI Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amepongeza wazazi wa wanafunzi wa shule ya wasichana ya masista wa Kikatoliki  Henry Gogarty iliyopo wilayani Arumeru kwa jitihada za kujenga majengo ya shule hiyo kwa hiari.

 Alisema mfano huo unapaswa kuigwa na wazazi wa shule nyingine.
 
Lowassa alisema hayo juzi kabla ya harambee ya ujenzi wa maabara na mabweni ya shule hiyo. Alisema kuwa wazazi wengine wanapaswa kuiga mfano huo.
 
 Alisema pongezi  anazotoa ni za dhati, zinazopaswa kuigwa na wazazi wengine kwani katika harambee nyingi alizowahi kufanya, hajawahi kuona wazazi wanaoweza kujitoa kwa kiasi kikubwa kuchangia harambee na maendeleo ya shule.
 
 "Hawa wazazi wanapaswa kupongezwa na mfano huu unapaswa kuigwa katika shule zingine, kwani wengi wamekuwa wakitaka kuchangiwa tu, tofauti na hapa wazazi wanachanga wenyewe hivyo wanapaswa kupewa nguvu kubwa,’’alisema.
 
 Pia, Lowassa alilisifu shirika la masista wa Mkoa wa Kilimanjaro kwa jitihada zake za kuendeleza elimu hapa nchini na nje ya nchi.
 
  Alisema na kuisifu shule hiyo katika kufanya vizuri katika mitihani yake ya Taifa. Aliwataka walimu kuendelea na moyo huo ili shule hiyo iweze kuongoza kitaifa.
 
 Mkuu wa Shule hiyo, Bernada Moshi alisema shule hiyo ilianzishwa mwaka 2011 na inakabiliwa na changamoto kubwa za uhaba wa mabweni kwa ajili ya wanafunzi wa kike na maabara.
 
 Moshi alisema lengo ni kukusanya Sh milioni 250 kwa kujenga majengo ya mabweni na maabara. Alisema lengo kuu la shule hiyo ni kutoa elimu bora na maadili kwa mtoto wa kike, ambaye ni nguzo muhimu katika maendeleo ya familia na jamii.  

Katika harambee hiyo, jumla ya Sh196,493,350 zilichangwa, huku fedha taslimu zikiwa Sh 120,863,350 na ahadi Sh 75,630,000.
 
 Lowassa pamoja na rafiki zake walitoa Sh milioni 10 na kompyuta mbili.

0 comments:

Post a Comment