Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, March 19, 2013

Nancy Sumari azindua kitabu cha kusaidia wanawake

Akimuonesha kitabu hicho Professor Esther Mwaikambo

                  Faraja Kotta Nyarandu akitoa maoni yake kuhusiana na kitabu hicho
                                        Wanafunzi wakifuatilia kwa umakini wa hali ya juu
                                                Hao ndio wahusika wakuu wa kitabu hicho
                                                                       Nancy na Faraja
                                                                 Nancy akisaini kitabu chake
                                              Wakaanza kukisoma wanafunzi
                          Ilikuw furaha kwa wanafunzi

MLIMBWENDE wa Tanzania mwaka 2005 Nancy Sumari jana alizindua kitabu kiitwacho Nyota Yako alichokitunga mwenyewe chenye ujumbe wa kuwahamasisha wasichana masuala mbalimbali yanayowahusu ikiwa pamoja na kutoa ujumbe mbalimbali wenye kulenga kusaidia kuwaepusha na hatari mbalimbali.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho Nancy alisema kuwa akiwa kama mlimbwende pia mwanaharakati wa haki za wasichana ameona kuwa kuna kila sababu ya kuzungumza na wasichana wa Tanzania nzima kwa njia hiyo.

Alisema kuwa kitabu hicho chenye kurasa 26 kinaelezea nafasi ya mwanamke katika jamii ya kitanzania, uwezo wa mtoto wa kike, Umuhimu wa namna ya kujithamini, kuweka malengo, ndoto na maazimio, kujiamini kujiendeleza kimalengo.

Katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na wadau wengi wa elimu nchini pia uluhudhuirwa na mshindi wa Tuzo ya JMartin Luther King Esther Mwaikambo ambae pia mbali na kumpongeza Nancy aliwasihi wasichana wenye mafanikio nchini kuwa na shauku ya kuwasaidia wasichana wengine wenye kutaka kutumiza ndoto zao.
Mwisho

0 comments:

Post a Comment