Help Children
Love them
Saidia Watoto

Friday, August 30, 2013

Diamond afundisha kivitendo suala la upendo na heshima

Watu wengi walihudhuria uzinduzi huo


Akampatia funguo zake


Tukaenda kwenye gari

Hata wapishi walimpongeza




MSANII wa muziki wa kizazi kipya Nasib Abdul, Diamond  juzi alimkabidhi gari mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini aliyestaafu muziki hivi karibuni Muhidin Gurumo.

Diamond alimkabidhi mzee huyo gari hilo wakati wa hafla ya kuzindua video ya wimbo wake mpya uitwao My Number One.

Blog hii limelichukulia tukio hilo kuwa ni kama elimu ambayo Diamond ameamua kuitoa kwa watu hasa jamii ya wanamuziki wenzake ya kuheshimu na kuendeleza maisha ya wengine.


Mzee Gurumo ametumikia bendi nyingi ambazo hazijawahi hata kumsaidia mabati ya kujengea nyumba lakini kwa Diamond ameonesha zaidi ya mfano kwa mzee huyo 
Diamond baada ya kuzungumzia video yake hiyo hususan katika suala la gharama na changamoto aliyokutana nazo wakati wa kutengeneza video hiyo na ndipo alipomuita stejini mzee Gurumo.

Diamond alianza kwa kusema namna ambavyo amekuwa akimpenda na kumheshimu mzee Gurumo na kisha akaendelea kusisitiza kuwa amesikitishwa na namna mzee huyo anavyohangaika kwa sasa.

Alimuita stejini na kisha akamkabidhi funguo wa gari hali iliyopelekea wageni waalikwa kupiga kelele za kushangilia baada ya kuguswa na tukio hilo.

Bada ya hapo Diamond alimshika mkono mzee huyo na kisha wakiongozana na wageni waalikwa kwa pamoja walitoka nje na kwenda kuliangalia gari hilo.

Baada ya hapo wageni hao pamoja na Diamond walirudi tena ndani na kuendelea na ratiba kama kawaida.

Awali akizungumzia Video yake hiyo alisem akuwa imemgharimu zaidi ya milioni 50 ambapo aliitengenezea nchini Afrika Kusini.

Ni Video nzuri na ya aina yake ambayo imegusa mazingira halisi ya maisha ambayo alikuwa akiyaimba katika wimbo wake huo wa mapenzi.
Mwisho

0 comments:

Post a Comment