Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, August 20, 2013

Vyuo vyatakiwa kupitia mitaalam yao



MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imevitaka vyuo vya elimu ya juu nchini, kuweka utaratibu wa kuipitia mitaala yao hasa katika eneo la mawasiliano iweze kwenda sanjari na kasi ya ukuaji wa teknolojia nchini.


Msemaji wa Mamlaka hiyo, Innocent Mungy,  alisema hayo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa progamu tatu za uzamili uliofanywa na Chuo cha Uhasibu cha Arusha (IAA) kwa kushirikiana na Chuo cha  Galgotias cha nchini India.


Mungy alisema taifa linapozidi kupiga hatua kimaendeleo katika nyanja za mawasiliano, ni vizuri vyuo vyote na hasa vya elimu ya juu vikaweka mkazo kuhakikisha  vinapitia vyema mitaala ya ufundishaji kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia yaliyopo.


“TCRA imekuwa ikitoa udhamini kwa wanafunzi mbalimbali katika fani za teknoham

a, hii  ni kwa lengo la kuwahamasisha zaidi ili waweze kutilia mkazo katika eneo hilo na hivyo kuongeza idadi ya wataalamu nchini,” alisema Mungy.

Akizungumzia uzinduzi wa programu hizo za uzamili katika masuala ya Kompyuta, Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Profesa Johannes Monyo, alisema malengo ya chuo ni kuongeza idadi ya wataalamu katika fani hizo ili kuleta ushindani kimataifa.

0 comments:

Post a Comment