Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, August 18, 2013

Elimu ya kujitambua katika kutumia fursa yatolewa Kigoma

  1. Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya na mfanyabiashara,Ambwene Yesaya a.k.a AY akitoa ushuhuda wake na mifano mbalimbali  katika Semina ya Fursa,kuhusiana na fursa alizozipata na kuzifanyia kazi,na kumpelekea mafanikio aliyonayo mpaka sasa.



  1.  Mkali wa kughani mashairi hapa nchini,Mrisho Mpoto akifafanua jambo mbele ya wakazi wa mji wa kigoma,alipokuwa akiielezea mada mojawapo iliyohusiana na fursa mbalimbali.

  1. Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group,Ruge Mutahaba akimkaribisha mgeni rasmi wa semina hiyo,Mh Issa Machibya wakati wa uzinduzi wa semina ya Fursa,kulia kwake ni msanii mahiri wa kughani mashairi hapa nchini,Mrisho Mpoto ambae pia likuwa ni mmoja wa watoa mada kuhusiana na suala zima la Fursa.
  2.  
  3. Habari kamili
  4.  
  5. Kampuni ya simu za mkononi ya Zantel imeunga mkono juhudi za kusaidia vijana kuchangamkia fursa, kampeni inayoendeshwa pia kupitia tamasha la Fiesta.

    Kampeni hizo ni za kuhamasisha vijana kuchangamkia fursa zilizopo nchini ambapo zitaendana na tamasha la Fiesta linaloendeshwa kwenye zaidi ya mikoa 13 kwa kushirikiana na Clouds Media Group.

    Katika kila mkoa kampeni hiyo itakuwa ikifanyika siku moja kabla ya siku ya tamasha la Fiesta.

    Kwa mkoa wa Kigoma alikuwepo msanii Mrisho Mpoto pamoja na Ambwene Yesaya, AY ambao kwa pamoja walikuwa kivutio katika kuhamasisha vijana kujituma na kuwa wabunifu katika kutumia fursa katika nyanja mbalimbali ikiwamo ya muziki.


    Mada zitakazojadiliwa kwenye semina hizo ni pamoja na ubunifu, ujasiriamali, Uongezaji thamani kwenye bidhaa au shughuli yoyote unayofanya pamoja na kujenga ushirikiano, uwekezaji pamoja na lugha.

    Akizungumzia semina hizo, Afsa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan, amesema kampuni yake imekuwa msitari wa mbele katika kuwawezesha vijana, na kwa semina hizi wanaamini vijana wengi watapata nafasi ya kuzitambua na kujifunza.

    ‘Tanzania ina fursa nyingi sana kwa vijana, na sisi Zantel tunaamini nafasi hii itakuwa muhimu kwa vijana kujifunza na kutambua fursa zilizopo kutoka kwa wataalamu mbalimbali’ alisema Khan.

    Naye Mkurugenzi wa Utafiti na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, alisema nchi ya Tanzania ina fursa nyingi lakini tatizo limekuwa ni namna ya kuzitumia fursa hizo.

    ‘Tumeandaa semina hizi kwa kutambua tatizo kubwa lilipo kwenye jamii yetu, umaskini na ukosefu wa ajira kwa vijana, jambo ambalo semina hizi zitaenda kutatua’ alisema Mutahaba.

    Mojawapo wa wazungumzaji kwenye semina hizo atakuwa Mrisho Mpoto, mwakilishi wa mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), Ruge Mutahaba pamoja na wageni waalikwa mbalimbali.

    Kwa mwaka huu semina hizo zimeanzia mkoa wa Kigoma, katika Ukumbi wa Kibo Hall Park, na mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya.




0 comments:

Post a Comment