Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, August 20, 2013

Viatu 590,000 vyagaiwa bure kwa wanafunzi

CHAMA  cha Msalaba Mwekundu Tanzania, kimegawa bure jozi 590,000 kwa wanafunzi wasio na uwezo kuvinunua katika mikoa saba nchini .

Ugawaji huo ulianza jana baada ya Rais wa Chama hicho, George Nangale kuzindua mradi wa viatu kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Dar es Salaam.


Akizungumza  wakati wa uzinduzi huo, Nangale alisema viatu hivyo vyenye thamani  ya jumla ya tshs builioni 2.4 vimetolewa kwa chama hicho na kampuni ya Tom Shoes ya Marekani ili vigawiwe kwa wanafunzi wahitaji bila malipo yoyote.


“ Tumepokea kontena 50 za raba hizo na tayari zimekwisha tawanywa kwenye mikoa husika ikiwemo Dar es Salaam, Pwani na Kilimanjaro  tayari kuanza kupewa walengwa mara baada ya kuzindua mradi huu muda ( jana),” Nangale alisema.


Kwa maelezo yake, kampuni ya Tom Shoes imelenga kuwalinda wanafunzi hao na maradhi ya safura, minyoo na mengine yanayotokana na kukanyaga ardhini bila viatu.


“Katika Afrika Kenya, Malawi, Zambia zilipewa msaada kama huo na sasa  Tanzania imekumbukwa, watatuletea jozi nyingine milioni moja kabla ya mwisho wa mwezi ili tufikie mikoa yote bara, mikoa yote mitano ya Zanzibar iko kwenye hesabu ya jozi 590,000,” alisema.


Meneja mradi wa chama hicho alisema kampuni hiyo itaendelea kutoa msaada wa viatu kwa wanafunzi Tanzania iwapo masharti ya kuviuza na kutogawa kwa upendeleo yatazingatiwa . 


Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Afya wa chama hicho,  Bertha Mlay  msaada huo ni endelevu kwa miaka mitatu .
mwisho

0 comments:

Post a Comment