Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, September 18, 2012

Mengi atoa somo la biashara kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini


 
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo Vya Habari Nchini            (MOAT) Regnard Mengi akipokea hati ya usajili ya Chama Cha Kuweka na Kukopa cha Wahariri, Wahariri Development Saccos kutoka kwa mwenyekiti  wa saccos hiyo Gogfrey Shogolo anayeshuhudia katikati ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Absolom Kibanda na kushoto ni ofisa wa  wa Ushirika kutoka Manispaa ya Ilala Stanslaus Mwansao (Picha na Evance Ng’ingo)




WAHARIRI pamoja na Waandishi wa Habari nchini wametakiwa kutambua kuwa ni jukumu lao kuinua kipato chao na hakuna mtu mwingine mwenye jukumu hilo.

Wito huo ulitolewa juzi na Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini (MOAT)  Reginard Mengi katika viwanja vya Karimjee wakati akizindua Chama cha Kuweka na Kukopa cha Wahariri, Wahariri Development Saccos.

Mengi alisema kuwa iwpao wahariri wakijiendeleza kimaisha wanaweza kuwa huru katika kufanya maamuzi yao wenyewe kulingana na maadili ya kazi zao bila kurubuniwa na watu wengine. 

Alisema kuwa Saccos ni njia mojawapo ya kuinua kipato chao hivyo aliwataka kuitumia vema kwa kuchukua mikopo yenye malengo ya kibiashara na ambayo wanaweza kuirudisha kwa muda unaotakiwa.

Pia aliwataka kuepuka migogoro ambayo inaweza kujitokeza kutokana na saccos hiyo huku akiwataka waitumie  kama chombo cha ukombozi wa maisha yao kwa kuimarisha wazo lao la biashara kabla ya kuchukua mkopo.

“ Kwanza ningependa muelewe kuwa pesa haina sura, hapa nikiwa na maana kuwa katika kuitafuta hakuna kuwa na mzaha nayo hakuna suala la aibu wala suala la kuogopa kuisaka” alisema Mengi.

“Natambua kuwa mtu huwezi kuwa mhariri mzuri huku ukikabiliwa na na shida mbalimbali,  sasa basi msikubali kuishia kupewa tu sifa kuwa nyinyi ni wahariri wazuri huku mkiwa mnakabiliwa na shida mbalimbali” aliongeza Mengi.

Aliahidi kuisaidia Saccos hiyo kwa kila hali ili iweze kutimiza ndoto yake na aliwaomba wahariri kukutana nae punde watakapokuwa wanahitaji msaada wake.

 Naye Mwenyekiti wa saccos hiyo Godfrey Shogolo alisema kuwa saccos hiyo ambayo ni kwa ajili ya wahariri inalenga kuinua maisha ya wahariri hao na kuongeza kuwa mchango wa kujiunga nayo ni shilingi 400,000/=
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini.

0 comments:

Post a Comment