Help Children
Love them
Saidia Watoto

Wednesday, May 15, 2013

HASA mradi imara wa kutoa elimu kwa watoto

Mwenyekiti wa Havillah Africa Sports Academy (HASA) Davis Mkony (katikati)wakati akipokea msaada wa mifuko 50 ya saruji iliyotolewa na duka la Mummy's lilipo Mlimani City anaekabidhi ni mwakilishi kutoka duka hilo Sam Mphungu alisema
Mwenyekiti wa Havillah Africa Sports Academy (HASA) Davis Mkony akiwa na wadau wengine wa Mradi huo wa Hasa.

Na Evance Ng'ingo
WAFANYABIASHARA na Makampuni mbalimbali yameombwa kuwekeza fedha zao kwenye michezo wa kusaidia ujenzi wa vituo mbalimbali vya michezo nchini.

Hoja hiyo ilitolewa jana na  Mwenyekiti wa Havillah Africa Sports Academy (HASA) Davis Mkony wakati akipokea msaada wa mifuko 50 ya saruji iliyotolewa na duka la Mummy's lilipo Mlimani City .
                                          
Msaada huo ni kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha michezo maalum kwa ajili ya watoto waishio mazingira magumu kwa lengo la kukuza vipaji vyao.

Mkony alisema kuwa makampuni makubwa yanatakiwa kutambua kuwa kwa kuwekeza michezo kwa watoto wadogo hususan wa mitaani itasaidia kuimarisha mazingira mazuri ya biashara zao.

Alisema kuwa michezo ndio njia pekee ya kuwanusuru watoto hao kujiingiza katika majanga mbalimbali pindi wawapo wakubwa.

Akizungumzia maandalizi ya mradi  huo wa michezo kwa watoto  unaojengwa katika eneo la Mkuza Mkuranga, Mkonyi alisema kuwa mradi huo unatarajia kukamilika Novemba mwezi huu.

Alisema kuwa unahusisha ujenzi wa majengo makubwa mabweni ya kulala watoto hao pamoja na madarasa.

Alisema kuwa tayari wameshanunua hekari 400 ambazo zinamilikiwa na mradi huo na kwa sasa wameanza mchakato wa kulitayarisha vema eneo hilo.

" Najua michezo ni kiwanda ambacho kinaweza kuzalisha mamilioni ya fedha kutoka kwa watoto na nchi inaweza kutambulika kimataifa zaidi kupitia michezo hiyohiyo" alisema Mkony.

Alifafanua kuwa mradi huo unalenga pia kusambaa nchi nzima kwa lengo la kutafuta na kuendeleza vipaji vya watoto hao na kuongeza kuwa ndani ya miaka ijayo watoto hao wanaweza kufika katika anga la kimataifa zaidi.

Naye mwakilishi kutoka duka hilo Sam Mphungu alisema kuwa likiwa kama duka kubwa la mavazi linatambua umuhimu wa michezo katika kusaidia kukua kwa jamii.

" Tulipopata maombi kutoka kwa hawa watu wa HASA kutuomba tusaidie harakati zao hizi za kukuza vipaji vya watoto tulichukua uamuzi wa kuwasaidia kwa moyo mmoja na tutaendelea kufanya hivyo" alisema Mpunghu.
Mwisho

0 comments:

Post a Comment