Help Children
Love them
Saidia Watoto

Monday, February 18, 2013

VEPK yaomba ushirikiano kuimarisha elimu nchini


SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Village Education Project Kilimanjaro(VEPK) limeiomba serikali na wadau mbalimbali kushirikiana ili kuhakikisha wanafunzi wa shule ya msingi wanajifunza na kuielewa lugha ya Kiingereza ili waweze kufanya vizuri wanapojiunga na elimu ya Sekondari.

Aidha shirika hilo limeomba waalimu wanaofundisha katika shule za msingi wasaidiwe kwa kuwezeshwa vifaa na kuendelezwa kielimu kwa kuwa wao ndo kitovu cha maendeleo ya elimu nchini.

Mkurugenzi wa VEPK, Katy Allen aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu tatizo linalochangia wanafunzi kutofanya vyema katika masomo yao hasa katika mitihani ya Taifa.

Alisema kuwa pamoja na kwamba wapo wanafunzi wengi ambao wanamaliza elimu ya msingi hawakijui kiingereza lakini pia wapo waalimu wengi ambao hawaijui lugha hiyo  na wanahitaji kusaidiwa.

Alisema kutokana na changamoto hiyo shirika hilo limeandaa vitabu kwa ajili ya darasa la tatu hadi la saba vitakavyosaidia walimu na wanafunzi kujifunza lugha hiyo lakini changamoto wanayokabiliana nayo ni jinsi ya kuviingiza katika mtaala.

Alisema wameshazungumza na viongozi mbalimbali na tayari vitabu hivyo vimeshafanyiwa majaribio na hivyo kuiomba serikali iviangalie upya ili kuweza kusaidia wanafunzi kuielewa lugha ya kiingereza.
Kwa Upande wake mratibu wa shirika hilo, Dilly Mtui alisema kuwa shirika hilo limelenga kukifanya kiingereza kuwa lugha rahisi ili kila mtu akifahamu.

“Tatizo letu kubwa ni kwamba hatupendi mabadiliko, tunajenga msingi wetu kwa kutumia matope mwishowe nyumba inaanguka, hivyo vitabu hivi ni dawa ya kukifanya kiingereza kuwa lugha rahisi” alisema.
Mwisho

0 comments:

Post a Comment