Help Children
Love them
Saidia Watoto

Friday, February 8, 2013

Michuano ya Vyuo Vikuu Afrika Mashariki yaanza leo

Wanafunzi wa Mkwawa wakifurahia

Wanafunzi wa Uganda wakihamasishana

Wadau  kutoka Zantel wakifuatilia mashindano hayo



Waziri wa vijana, utamaduni na michezo, Fenella Mukangara akisalimiana na Afsa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan wakati wa uzinduzi wa michezo ya vyuo vikuu Afrika Mashariki. Katikati ni Meneja Mkuu wa mawasiliano wa Zantel, Awaichi Mawalla.Zantel ni mojawapo wa wadhamini wa michuano hiyo.

Habari Kamili

 
WANAFUNZI wa vyuo vikuu vya Afrika Mashariki wametakiwa kuwa vinara katika kuhamasisha amani na usalama kwa njia ya michezo katika nchi zao.

Wito huo ulitolewa jana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fennela Mukangara wakati akifungua michuano ya siku tano michezo mbalimbali ya vyuo vikuu vilivyopo katika nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki iliyoanza jana katika viwanja vya Chuo Kikuu Dar es salaam..

Fennela  aliwataka wanafunzi hao wanaoshiri michezo hiyo kuhakikisha kuwa mbali na kushiriki michezo hiyo pia wanawajibu wa kuhakikisha kuwa wanajadili masuala mbalimbali ya amani na namna ya kuidumisha.

Pia Fenella aliwataka wanafunzi hao kuwa mabalozi wazuri katika kudumisha jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kujadiliana namna mbalimbali ya kudumisha ushirikiano huo.

Alisema kuwa wanaweza kubadirishana mawazo ya namna ya kuboresha mazingira katika sekta mbalimbali ya jumuiya ya Afrika Mashariki na aliwataka kuhakikisha kuwa wanakuwa mfano bora kama vijana katika kufanikisha hilo.

“ Mkiwa kama vijana mnalo jukumu kubwa kuhakikisha kuwa mnatumia michezo hii katika kudumisha amani na upendo katika jumuiya kwa kuwa kama mnavyofahamu kuwa michezo ndio moja kati ya njia za kipekee zinazowaweka pamoja wanajamii na hivyo nyie mkiwa kama vijana huu ni wakati wenu kujadilia masuala ya amani pia” alisema Fennela.

Kwa upande wake Ofisa Biashara Mkuu wa kampuni ya mkononi ya Zantel inayodhamini michuano hiyo  Sajid Khan alisema kuwa kampuni hiyo inatambua umuhimu wa michezo katika vyuo vikuu kwa kuwa wanafunzi hao ndio wanakuja kuwa wafanyakazi wa baadae hivyo wakijiandaa kimichezo wkaiwa vyuoni inaongeza afya na utendaji unakuja kuwa mzuri wakianza kazi.

Naye Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Yunus Mgaya alisema kuwa michezo hiyo iliyoanza jana itaendelea hadi februali 12 katika viwanja vya chuo hicho.

Alisema kuwa michuano hiyo inahusisha michezo mbalimbali kama vile riadha, kuogolea, mpira wa miguu, pete, kikapu netiboli na michezo mingine.

Alisema kuwa kwa hapa Tanzania vyuo vilivyoaliwa ni saba huku Uganda vikiwa vyuo 17 na Kenya vyuo 17 pia lakini hata hivyo gaezti hili lilishuhudia vyuo vya kutoka hapa nchini ni Chuo Kikuu Huria na Chuo Kikukuu cha Mkwawa peke yake vikiwa vimewasili katika viwanja hivyo. 

0 comments:

Post a Comment