Help Children
Love them
Saidia Watoto

Monday, July 23, 2012

Suala la elimu lilivyogusiwa leo bungeni


Serikali imeongeza kiwango cha alama za kuwachagua wanafunzi wanaotakiwa kwenda kujiunga na elimu ya vyuo vya ualimu.

Awali ilikuwa ni mhitumu wa kidato cha nne mwenye alama division 4.28 alikuwa anaweza kujiunga na elimu ya ualimu lakini kwa sasa ni wale wenye division 4.27 tu.

Hatua hii ni nzuri kwa kuwa inawapatia nafasi wanaojiunga na ualimu kuwa katika mazingira mazuri ya kuwafundisha wanafunzi kwa kuwa nao wanakuwa ni wenye uelewa zaidi.

Hayo yalisemwa leo na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Shukuru Kawambwa wakati akijibu maswali bungeni.

Tutaendelea kuwajulisha yanayojili bungeni Dodoma katika sekta hii ya elimu ambayo ni muhimu kabisa hapa nchini.

0 comments:

Post a Comment