Help Children
Love them
Saidia Watoto

Monday, July 16, 2012

Pazia la uchangiaji wa ujenzi wa hosteli za wasichana lilipofunguliwa rasmi huko KIbaigwa Dodoma

 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii na Watoto Ummy Mwalimu akicheza ‘kwaito” na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kibaigwa katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ujenzi wa mabweni 30 nchi nzima kwa mtoto wa kike
 
Waziri kivuli wa Elimu na mbunge wa viti maalumu kupitia CHADEMA Susan Lyimo akiongea katika hafla ya uchangiaji wa mabweni. Katika hafla hiyo jumla ya shilingi 37,214,000/= zilipatikana ikiwa ni ahadi pamoja na fedha taslim.
 
Mgeni Rasmi, Waziri kivuli wa Elimu na mbunge wa viti maalumu kupitia CHADEMA Susan Lyimo akipokea mkasi kutoka kwa Mwenyekiti wa bodi ya TEA Dkt Naomi Katunzi kwa ajili ya kuzindua rasmi harambee ya ujenzi wa mabweni 30 kwa ajili ya watoto wa kike wa sekondari nchini.
 Naibu Spika wa Bunge na Mbunge wa Kibaigwa Job Ndugai Akivuta utepe uliokatwa na mgeni rasmi Mh. Suzan Lyimo huku tukio hilo likishangiliwa na viongozi mbalimbali wa serikali na TEA

Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania Sylvia Lupembe Gunze (kushoto) akijadiliana mambo mawili matatu na diwani wa Kibaigwa Richard Kapinye na Afisa Elimu Taaluma wa Kongwa bi Emilia Litunguru.

0 comments:

Post a Comment