Help Children
Love them
Saidia Watoto

Tuesday, July 17, 2012

Hassan Maajar Trust (HMT) yakabidhiwa milioni 23 na Tigo kununulia madawati 745

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa (kushoto), akikadidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. mil 26, Mwenyekiti wa Kamati ya Harambee wa Taasisi ya Hasaam Maajar Trust (HMT), Dk Sinare Yusufu, kwa ajili ya kununa madawati 745 yatakayogawiwa katika shule za msingi zilizopo wilaya ya Njombe na Makete. Anayeshuhudia katikati ni Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Andrew Hogdson ambayo imetoa Fedha hizo zilizotokana na michange ya matembezi ya hiari ya ‘Tigo Tuchange.’

 Na Mwandishi wa Elimubora

Tigo imekabidhi  fedha zilizopatikana katika mfuko wa matembezi ya hiari ya Tigo Tuchange kwa Hassan Maajar Trust ( HMT),  ni mpango wa muda mrefu uliyoundwa ili kuboresha mazingira ya kusoma mashuleni kwa kugawa madawati katika shule mbalimbali za wahitaji.

Sherehe za makabidhiano zilihudhuriwa na Mheshimiwa Dr. Shukuru Kawambwa , waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi, wanachama wa HMT , mwandamizi mtendaji wa Tigo na wafanyakazi.

“Moja ya lengo letu ni kuhakikisha wanafunzi wana vifaa vya kujifunzia na mazingira tulivu ya kusomea”alisema Mh. Dk  Kawambwa. Tunawapongeza Tigo kwa kutoa ushirikiano mzuri kwa raia na tunaomba makampuni mengine kuisaidia serikali katika kuleta maendeleo endelevu  katika nchi” hii alisema.

Hundi ya Sh. 26, 000,000 iliwasilishwa  kwa niaba ya Tigo na Andrew Hudgson,Kaimu meneja Mkuu , kwenda kwa Mkurugenzi mtendaji wa HMT, Zena M Tenga. Fedha zilipatikana kwa njia ya  ukusanyaji wa Tigo rusha top ups iliyofanywa mida ya saa 5 asubuhi na 12 jioni siku ya tarehe 3 March.Wateja ambao waliweka muda wa mawasiliano kwa muda huo walitumia muda wao wa mawasiliano wakati kuenda kiasi kama hicho kwa mpango huo

Mpango huu ni kulingana na dhamira yetu  ya kushirikiana na jamii  katika kuelewa mahitaji ya jamii zinazotuzunguka maeneo tunayofanyia biashara, ili kutengeneza mchango mzuri na endelevu katika kuwainua” alisema Bw.Hudson “ Tungependa kuwashukuru tena wote kwa mchango wenu katika mfuko huu muhimu’ alisema

Chini ya mradi wa shule 5 (tano) kutoka wilaya mbili (Njombe & Makete) zilizoko wa  mkoa wa Iringa zitapokea madawati kama ifuatavyo: Maendeleo: 135, Umoja: 196,Kumbila: 200, Makonde: 152 na  Mbela: 37.

Shule zilichaguliwa kulingana na kuwepo kwa haja kubwa zaidi. Mradi hautafaidhisha tu shule na wanafunzi, bali kwa kununua madawati ndani ya nchi kutasaidia katika kutengeneza nafasi za ajira kwa wafanyabiashara na vijana katika maeneo hayo na hivyo kuleta maendeleo ya kiuchumi katika sehemu hizo.

“Ningependa kutoa shukrani  za dhati kwa niaba ya HMT kwenda kwa Tigo katika kushiriki kwao kuwapatia watoto hawa  fursa itakayowafanya  ya kuweza kujitegemea na kwa upande wa kuwawezesha na kuwaruhusu wale kuhitaji misaada yao katika siku zijazo,” Bi. Tenga. “ Mwanafunzi anaposoma katika mazingira mazuri na tulivu wanakuwa na umakini zaidi na kuzalisha matokeo mazuri zaidi na hyivyo kupata maisha bora baadaye, na kwa  kupitia miradi endelevu ya namna hii tunaweza kuleta jitihada kubwa katika kuleta maendeleo ya uchumi  ndani ya jamii, “ alisema.


0 comments:

Post a Comment