Help Children
Love them
Saidia Watoto

Sunday, July 22, 2012

Majaji wa EBSS waomboleza msiba wa meli Zanzibar, pia waendeleza somo la muziki

 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano wa Zantel Awaichi Mawalla kulia akiwa pamoja na majaji wa EBSS 2012 wakiwa wamesimama kuomboleza msiba wa meli wa Zanzibar
 Washiriki nao wakiwa wamesimama kuomboleza msiba huo
Baadae waliendeleza zoezi la kufuatilia vipaji ambapo pia walitoa elimu kwa washiriki waliojitokeza katika usaili mkoani hapo.

Na Mwandishi wa elimuboratanzania, Mbeya
WASICHANA wawili pamoja na wavulana watatu wamechaguliwa kuuwakilisha mkoa wa Mbeya katika fainali za taifa za shindano la kusaka vipaji la Epiq Bongo Star Search (EBSS 2012)

Washindi hao ambao kwa sasa majina yao wala picha zao havitakiwi kutangazwa kwenye vyombo vya habari walionesha uwezo mkubwa katika kuimba nyimbo mbalimbali.

Akizungumzia vipaji vya Mbeya jaji mkuu wa EBSS 2012 Ritha Paulsen alisema kuwa washindi hao wametoka katika kundi la vijana zaidi ya 500 waliojitokeza mkoani hapa.

Alisema kuwa mbali na mkoa wa Mbeya kusifika kwa kuimba nyimbo za injili lakini wameweza pia kuonesha uwezo katika nyimbo nyingine mbalimbali za kidunia.

Alisema kuwa wamefanikiwa kuwafundisha muziki vijana wengi ikiwa pamoja na kuwaelimisha juu ya namna ya kutoka zaidi sit u kimuziki bali pia hata katika masuala mengine ya sanaa.

“ Mbali na washiriki kuja kwa nia ya kuimba lakini pia wapo ambao wamegundulika kuwa na uwezo wa kuigiza na kufanya aina nyingine za sanaa ambazo tumewaelekeza kuzifanya” alisema Ritha.

Alisema kuwa tofauti na mikoa mingine katika mkoa wa Mbeya ameshuhudia akinamama wenye vipaji wakishiriki kuimba kitu ambacho alisema kuwa ni tofauti na mikoa mingine walioenda.


0 comments:

Post a Comment