Help Children
Love them
Saidia Watoto

Thursday, October 10, 2013

Fedha za mikopo kwishnei


KITENDO cha wanafunzi kukosa mikopo kwa muhula wa mwaka 2013 na 2014 inatokana na kuisha na hivyo kuwa chanzo cha baadhi ya wanafunzi kukosa mikopo kwa muhula wa masomo wa mwaka 2013/14.
 

Jana baadhi ya wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dodoma Chuo Kikuu wa Iringa, Chuo cha Kiislamu cha Morogoro walikusanyika karibu na Ukumbi wa habari maelezo baada ya juhudi za kwenda Ikulu kugonga mwamba.





Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilitenga sh bilioni 306 kwa ajili ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya juu nchini, ikiwa ni pamoja na waombaji wapya na wanafunzi wanaoendelea na masomo.


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Bodi hiyo, Cosmas Mwaisobwa alisema jana wanafunzi waliopata ni kutokana na fedha walizokuwa wametengewa kwa kazi hiyo.


“ Wengine wamekosa kwasababu fedha zimekwisha, tumekopesha mpaka senti ya mwisho ilipoishia ndio ukawa mwisho.Na hili ni kamaida kwa watu kukosa kutokana na uhaba wa fedha,” alisema na kuongeza kuwa kama kunabaadhi ya watu wanaandamana kwa hilo itakuwa ni unaharakati wao.



Akizungumza kwa niaba ya wenzao, Athuman Mohamed amelalamikia hatua ya kukosa mikopo na kudai kuwa wengi waliokosa ni yatima na wasi na uwezo wa kujisomesha.

0 comments:

Post a Comment