Help Children
Love them
Saidia Watoto

Monday, May 7, 2012

Wasanii Mabalozi wa Malari waendeleza elimu kwa wanajamii dhidi ya ugonjwa huo

 Walishikana mikono kuashiria ushirikiano katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo
Wasanii wa Tanzania House of Talent (THT) wakitumbuiza katika uzinduzi wa kampeni ya Night Watch inayolenga kuhamasisha matumizi ya vyandarua nyakati za usiku
Balozi wa kujitolea wa vita dhidi ya ugonjwa wa Malaria Mwasiti Almasi akimkabidhi fulana yenye ujumbe wa mapambano ya vita dhidi ya Malaria Michael Finlay wa ExxonMobil ambao ni wadau wakubwa wa mapambano dhid ya Malaria ( Na Mpigapicha Wetu)
Diamond alikuwapo kuwapa tafu.

Na Mwandishi Wetu
WASANII ambao ni mabalozi wa vita dhidi ya Malaria wametakiwa kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa huo ili kuinusuru jamii kubwa ya wanajamii.

Wito huo ulitolewa juzi na Meneja wa Mradi wa Kitaifa wa Kudhibiti Malaria (NMCP) Dk Ally Mohamed wakati akizindua kampeni mpya ya kupambana na ugonjwa wa Malaria iitwayo Night Watch inayoratibiwa na mradi wa Zinduka na kuwashirikisha mabalozi hao.

Dk Mohamed alisema kuwa wasanii wanaweza kutumia nguvu ya sanaa katika kuielimisha jamii juu ya ugonjwa wa Malaria hasa kwa kuondoa dhana potofu ambazo zinarudisha nyuma juhudi za serikali katika kupinga ugonjwa wa Malaria.

Alisema kuwa kampeni hiyo mpya ya Night Watch ambayo inawahamasisha wanajamii kutumia vyandarua nyakati za usiku ni kampeni nzuri na yenye kuleta tija katika vita dhidi ya Malaria.

Aliongeza kuwa  kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa maambukizi ya malaria nyakati za usiku  na hivyo aliwataka wasanii hao kutumia nafasi zao katika jamii kuhakikisha kuwa wanaitumia vema kampeni hiyo ya Nighwatch kuwakumbusha wanajamii kutumia vyandarua na masuala mengine muhimu.

“ Mradi NMCP unatambua mchango wa wasanii katika kupambana na ugonjwa wa Malaria ambapo kupitia kamepni hizi zinazofanywa mmewezea kuongeza uelewa wa watu juu ya ugonjwa huu na namna ya kupambana nao” alisema Dk Mohamed.

Wakizungumzia kampeni hiyo wasanii Mwasiti Almasi na Fid Q alisema kuwa wakiwa kama wasanii watatumia vipaji vyao katika kuhakikisha kuwa wanawakumbusha wanajamii umuhimu wa kutumia vyandarua.

Fiq Q alisema kuwa atahakikisha kuwa katika ngazi ya kifamilia wazazi na watoto wanatumia vyandarua kila usiku ili kuweza kuepuka maambukizi dhidi ya ugonjwa huo.

Pia hafla hiyo ilihudhuriwa na Michael Finlay wa ExxonMobil ambao kwa pamoja na African Barrick Gold ni wamekuwa wakidhamini shughuli mbalimbali za mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria.

Kampeni hiyo ya Nightwatch itaanza kutangazwa katika kituo cha redio cha TBC kuanza kesho (Jumatano) ambapo wasanii wanaoshiriki katika kampeni hiyo ni Diamond, Barnaba, Linah, Mwasiti, Bi Kidude na Professor J.
Mwisho

 




0 comments:

Post a Comment