Help Children
Love them
Saidia Watoto

Friday, May 18, 2012

Kipindi cha kuelimisha, kuburudisha na kuadabisha chaja EATV Alhamisi hii

 Mwendeshaji wa kipindi hicho Mboni Masimba akifafanua jambo kwa waandishi wa habari
 Mboni akiwa na Meneja Uhusiano wa kipindi hicho Shamim Mwasha wa 8020blog

   Waandishi wa habari wakichukua picha na maelezo kwa ajili ya kuwajuza wananchi.

Na Mwandishi wa Elimubora
KIPINDI cha Mboni Talk Show chenye kuburudisha, kuelimisha na kufundisha  ambacho kitaanza kuoneshwa Alhamis ijayo katika kituo cha East Africa Television.

Kipindi hicho kitarushwa na  Mboni Masimba ambae alisema kuwa vipindi vya Talk Show kwa sasa vinapendwa na kutazamwa na watu wengi zaidi kutokana na uvutiaji wake na mijadala mbalimbali ambayo inazungumzwa katika vipindi hivyo.

Akizungumzia kipindi chake Mboni alisema kuwa kipindi hicho kitakuwa na sehemu tano ambazo ni Ufunguzi, wakati wa maswali kutoka kwa mtangazaji kwa wageni na kutoka kwa hadhira kwenda kwa wageni, na pia kutakuwa na kipengele cha My dreams come true ambapo kipindi chake kitatoa misaada kwa watu wenye mahitaji mbalimbali na pia kutakuwa na Tamati.

Alisema kuwa kutokana na ukubwa wa Luninga ya East Africa Tv anahakika kuwa watu kutoka nchi za Afrika Mashariki wataburudika na kufurahishwa na kipindi hicho cha kipekee huku akiwataka wadau mbalimbali kutoa maoni yao mara baada kitakapoanza kurushwa.

“ Ni kwamba Tanzania kuna watu wa aina mbalimbali na wenye vipaji mbalimbali ambao wanatakiwa kuendelezwa na hapa ndipo nguvu ya Tv Talk Show inahitajika na mimi nitahakikisha kuwa kupitia kipindi change cha Mboni Show nitawafikiwa kila wenye kuhitaji msaada wa kuendelezwa kuwa wanafanyiwa hivyo” alisema Mboni 

Mboni aliwataka wasanii kutumia vipindi vya Talk Show kwa ajili ya kutangaza kazi zao sanaa ndani na nje ya nchi ikiwa pamoja na kuitangaza nchi ya Tanzania.

0 comments:

Post a Comment