<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000080;"><em><strong>Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari
 na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni 
(UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph, akielezea mantiki ya warsha ya wadau wa
 elimu kuhusu viwango vya umahiri wa Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya 
ualimu Tanzania iliyofanyika mjini Bagamoyo, mkoa wa Pwani mwishoni mwa 
juma.</strong></em></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Na Mwandishi Wetu, 
Bagamoyo</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi
 na Utamaduni (UNESCO), limesema litaendelea kushirikiana na serikali ya
 Tanzania kuhakikisha kwamba taifa linakuwa na wananchi wenye uwezo 
mkubwa wa kuvumbua na kutumia 
 elimu.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Kauli hiyo imetolewa na Ofisa wa Unesco 
 nchini Al Amin Yusuph wakati akizungumza na washiriki wa kongamano 
maalumu wa kupitia waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya
 ualimu.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Kongamano hilo ni moja ya mradi wa CFIT  wa 
UNESCO na serikali ya China wenye lengo la kusaidia serikali ya Tanzania
 kuimarisha umahiri wa wakufunzi na walimu kwa kuwawezesha kujua Tehama 
na kuitumia.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Mradi huo umelenga kuongeza uwezo wa vyuo vya
 walimu na teknolojia ya kisasa ya Tehama  na vifaa vyake ili kusaidia 
kujifunza na kufunza.</strong></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Ingawa kwa sasa vyuo vinavyofanyiwa kazi na 
mradi huo vipo viwili vya Tabora na Monduli vipo vingine vinane 
vinavyofunza walimu wa sayansi na hesabu ambavyo 
vitaingizwa.</strong></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000080;"><em><strong>Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa CFIT
 kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni 
(UNESCO), Faith Shayo akifafanua jambo kwa wadau wa kongamano la kupitia
 kitabu cha maf</strong></em><em><strong>unzo
 ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu nchini lililofanyika mjini 
Bagamoyo, Pwani mwishoni mwa 
juma.</strong></em></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Yusuph aliwataka wadau wanaoshiriki katika 
kongamano  ambalo lilitarajiwa kumalizika mwishoni mwa wiki kutekeleza 
wajibu wao kwa makini kwa kuwa Watanzania wanasubiri maelekezo yao 
kufanikisha utoaji wa elimu ya Tehama yenye kuleta mwelekeo mpya wa 
matumizi kwa kulenga  kuvumbua na kutumia elimu kwa manufaa ya 
taifa.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alisema UNESCO ipo tayari kuhakikisha kwamba 
Tanzania inazalisha wanafunzi ambao watakuwa na uwezo mkubwa katika 
Tehama ambao utaibua maendeleo 
endelevu.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong> “Si kutoa walimu wazuri tu bali kuwezesha 
jamii , wanafunzi na waliopitia mafunzo hayo kuwa na namna mpya ya 
kufikiri na kuvumbua vitu vipya vya kujiendelea na kuendeleza taifa” 
alisema Yusuph.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alisema kimsingi elimu inatoa asilimia 5 
lakini maisha yanatoa asilimia zilizobaki kama mtu atatumia vyema msingi
 wa maarifa aliyopewa.</strong></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000080;"><em><strong> Jaco Du Toit, kutoka ofisi za 
Unesco kanda ya Nairobi akiendesha majadiliano ya maboresho ya vipengele
 mbalimbali vya waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya 
ualimu"UNESCO ICT Competency Framework for Teachers in Tanzania" wakati 
wa kongamano hilo lililomalizika mwishoni mwa juma mjini 
Bagamoyo.</strong></em></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alisema lengo la mradi huo ni kuwezesha 
wanafunzi na walimu wao kuongeza maradufu uwezo wao katika 
elimu.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Naye Mratibu wa kitaifa wa Mradi Wa CFIT 
Kutoka UNESCO, Faith Shayo alisema kongamano hilo ni sehemu ya 
maandalizi ya mafunzo na matumizi ya maabara katika vyuo vya Monduli na 
Tabora katika kufunza Tehama ili kuboresha mafunzo na 
ufundishaji.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>“Leo tuko hapa Bagamoyo kwa ajili ya wadau 
kudiscuss ICT draft document (kujadili hati hii yenye draft ya mafunzo) 
ambayo ilipitiwa na watu  watano kabla ya kuikabidhi kwa Wizara ya Elimu
 “ alisema Faith.</strong></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alifafanua kwamba Mradi huo ambao awali 
ulifadhiliwa na  Benki ya Dunia na kukamilika mwaka 2011, haukuridhiwa 
kutumika hadi mwaka jana ulipokuja mradi wa CFIT ambao uliingizia 
upitiaji upya wa mradi huo na kuwezesha kuridhiwa kwa 
matumizi.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Naye  kiongozi wa timu iliyopitia awali 
katika mradi huo wa CFIT, Profesa  Ralph Masenge amesema wataalamu 
waliohusika na upitiaji huo kabla ya kongamano walitoka Chuo cha Ualimu 
Tabora na kile cha Monduli,Chuo kikuu huria Tanzania  na Chuo kikuu cha 
Dar es salaam.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alisema awali walipitia kuona mahitaji 
maalumu ya walimu kisha wakaja na mapendekezo ambayo sasa yanafanyiwa 
kazi .</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alisema matatizo mengi ya elimu Tanzania 
yanatokana na uhaba wa vifaa vya elimu  na ubora wa 
walimu.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alisema mradi huo utasaidia kutoa elimu bora 
kwa kuwa na walimu bora na vifaa bora kupitia 
Tehama.</strong></span></p>
<p 
style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Alisema mradi huo utasaidia  kuwezesha Tehama
 kutumiwa kama chombo cha kutumia wanafunzi hasa pale 
panapokosekana.</strong></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000000;"><strong>Profesa Masenge alisema hatua waliyofikia ni 
hatua ya matayarisho na kwamba ni matarajio yao kwamba wakishafikisha 
 hati hiyo kwa wizara masuala ya matumizi ya maabara yatakuwa 
yamekamilika.</strong></span></p>
<p
 style="text-align: center;"><span style="color: 
#000080;"><em><strong>Pichani juu na chini ni washiriki 
wakiwasilisha mawazo yao wakati kongamano likiendelea kujadili masuala 
mbalimbali ya kuboresha waraka 
huo.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Washiriki wa kongamano hilo wakifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa ikiwasilishwa.</strong></em></span></p>
KAWAIDA
Ofisa
 Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la 
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph, akielezea 
mantiki ya warsha ya wadau wa elimu kuhusu viwango vya umahiri wa Tehama
 kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu Tanzania iliyofanyika mjini Bagamoyo, 
mkoa wa Pwani mwishoni mwa juma.
Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo
SHIRIKA
 la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), limesema 
litaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kuhakikisha kwamba 
taifa linakuwa na wananchi wenye uwezo mkubwa wa kuvumbua na kutumia  
elimu.
Kauli
 hiyo imetolewa na Ofisa wa Unesco  nchini Al Amin Yusuph wakati 
akizungumza na washiriki wa kongamano maalumu wa kupitia waraka wa 
mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu.
Kongamano
 hilo ni moja ya mradi wa CFIT  wa UNESCO na serikali ya China wenye 
lengo la kusaidia serikali ya Tanzania kuimarisha umahiri wa wakufunzi 
na walimu kwa kuwawezesha kujua Tehama na kuitumia.
Mradi
 huo umelenga kuongeza uwezo wa vyuo vya walimu na teknolojia ya kisasa 
ya Tehama  na vifaa vyake ili kusaidia kujifunza na kufunza.
Ingawa
 kwa sasa vyuo vinavyofanyiwa kazi na mradi huo vipo viwili vya Tabora 
na Monduli vipo vingine vinane vinavyofunza walimu wa sayansi na hesabu 
ambavyo vitaingizwa.
Mratibu
 wa Kitaifa wa Mradi wa CFIT kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la 
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Faith Shayo akifafanua jambo kwa 
wadau wa kongamano la kupitia kitabu cha mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu nchini lililofanyika mjini Bagamoyo, Pwani mwishoni mwa juma.
Yusuph
 aliwataka wadau wanaoshiriki katika kongamano  ambalo lilitarajiwa 
kumalizika mwishoni mwa wiki kutekeleza wajibu wao kwa makini kwa kuwa 
Watanzania wanasubiri maelekezo yao kufanikisha utoaji wa elimu ya 
Tehama yenye kuleta mwelekeo mpya wa matumizi kwa kulenga  kuvumbua na 
kutumia elimu kwa manufaa ya taifa.
Alisema
 UNESCO ipo tayari kuhakikisha kwamba Tanzania inazalisha wanafunzi 
ambao watakuwa na uwezo mkubwa katika Tehama ambao utaibua maendeleo 
endelevu.
 “Si
 kutoa walimu wazuri tu bali kuwezesha jamii , wanafunzi na waliopitia 
mafunzo hayo kuwa na namna mpya ya kufikiri na kuvumbua vitu vipya vya 
kujiendelea na kuendeleza taifa” alisema Yusuph.
Alisema
 kimsingi elimu inatoa asilimia 5 lakini maisha yanatoa asilimia 
zilizobaki kama mtu atatumia vyema msingi wa maarifa aliyopewa.
 Jaco
 Du Toit, kutoka ofisi za Unesco kanda ya Nairobi akiendesha majadiliano
 ya maboresho ya vipengele mbalimbali vya waraka wa mafunzo ya Tehama 
kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu"UNESCO ICT Competency Framework for 
Teachers in Tanzania" wakati wa kongamano hilo lililomalizika mwishoni 
mwa juma mjini Bagamoyo.
Alisema lengo la mradi huo ni kuwezesha wanafunzi na walimu wao kuongeza maradufu uwezo wao katika elimu.
Naye
 Mratibu wa kitaifa wa Mradi Wa CFIT Kutoka UNESCO, Faith Shayo alisema 
kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya mafunzo na matumizi ya maabara
 katika vyuo vya Monduli na Tabora katika kufunza Tehama ili kuboresha 
mafunzo na ufundishaji.
“Leo
 tuko hapa Bagamoyo kwa ajili ya wadau kudiscuss ICT draft document 
(kujadili hati hii yenye draft ya mafunzo) ambayo ilipitiwa na watu  
watano kabla ya kuikabidhi kwa Wizara ya Elimu “ alisema Faith.
Alifafanua
 kwamba Mradi huo ambao awali ulifadhiliwa na  Benki ya Dunia na 
kukamilika mwaka 2011, haukuridhiwa kutumika hadi mwaka jana ulipokuja 
mradi wa CFIT ambao uliingizia upitiaji upya wa mradi huo na kuwezesha 
kuridhiwa kwa matumizi.
Naye 
 kiongozi wa timu iliyopitia awali katika mradi huo wa CFIT, Profesa  
Ralph Masenge amesema wataalamu waliohusika na upitiaji huo kabla ya 
kongamano walitoka Chuo cha Ualimu Tabora na kile cha Monduli,Chuo kikuu
 huria Tanzania  na Chuo kikuu cha Dar es salaam.
Alisema awali walipitia kuona mahitaji maalumu ya walimu kisha wakaja na mapendekezo ambayo sasa yanafanyiwa kazi .
Alisema matatizo mengi ya elimu Tanzania yanatokana na uhaba wa vifaa vya elimu  na ubora wa walimu.
Alisema mradi huo utasaidia kutoa elimu bora kwa kuwa na walimu bora na vifaa bora kupitia Tehama.
Alisema mradi huo utasaidia  kuwezesha Tehama kutumiwa kama chombo cha kutumia wanafunzi hasa pale panapokosekana.
Profesa
 Masenge alisema hatua waliyofikia ni hatua ya matayarisho na kwamba ni 
matarajio yao kwamba wakishafikisha  hati hiyo kwa wizara masuala ya 
matumizi ya maabara yatakuwa yamekamilika.
Pichani
 juu na chini ni washiriki wakiwasilisha mawazo yao wakati kongamano 
likiendelea kujadili masuala mbalimbali ya kuboresha waraka huo.
Washiriki wa kongamano hilo wakifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa ikiwasilishwa.