
SERIKALI imejipanga kuvikopa vyuo vikuu hapa nchini kwa ajili ya ada ya wanafunzi 1107 wa masomo ya kipaumbele waliokosa mkopo kutokana na fomu za maombi kuwa na dosari.
Akizungumza mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alisema hatua hiyo ni katika kutoa nafasi kwa wanafunzi hao hasa kutokana kompyuta kuwa na matatizo na baadaye kutoa fedha hizo kwa wanafunzi wengine.
“Ni...