
Chanzo gazeti la HabarileoWANAFUNZI kutoka vyuo 10 vya elimu ya juu nchini, wamewasihi wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kurejea ndani ya Bunge Maalumu la Katiba kuendelea na majadiliano.
Waliyasema hayo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jana jijini Dar es Salaam na kushutumu hatua yao ya kususia vikao vya Bunge hilo wakisema kitendo cha kueneza propaganda chafu kuhusu Katiba mpya nje ya ukumbi wa Bunge, ...