
Na Mwandishi WetuWIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imesema ni marufuku kukaririsha darasa, kuhamisha au kufukuza wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kwa kushindwa kufikisha wastani wa alama za ufaulu wa shule.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Wizara hiyo na kusainiwa na Kaimu Katibu Mkuu, Consolata Mgimba, ilisema Kumejitokeza tatizo la baadhi ya Shule za Sekondari zisizo za Serikali kukaririsha, kuwahamisha au kuwafukuza wanafunzi...