Walimu wawili wa shule ya Msingi Nzogimlole wilayani Nzega Mkoani Tabora wamejikuta katika wakati
mgumu baada ya kupigwa na kujeruhiwa vibaya na mzazi mmoja aliyetambulika kwa jina la Selemani Juma baada ya walimu hao kumurudisha shule mwanafunzi Shaabani Mziku kutokana na kuchanika kwa sare yake ya shule (bukta).
Mwandishi wa habari hii alifika katika shule hiyo ya Msingi Nzogimlole na kuzungumza na mwlimu mkuu msaidizi Emmanuel Josephat alisema...